Thursday 22 December 2016

Hatimaye Crystal Palace yamtupia virago kocha wao Alan Pardew baada ya kushindwa kuibeba timu



LONDON, England
KLABU ya Crystal Palace imemtupia virago kocha wao,  Alan Pardew huku klabu hiyo ikikamata nafasi ya 17 katika msimamo wa Ligi Kuu ya England.

Pardew aliteuliwa kuifundisha timu hiyo miaka mitatau na nusu iliyopita kuanzia Januari 2015 lakini kocha huyo mwenye umri wa miaka alijikuta akitupiwa virago baada ya timu yake kushinda mchezo mmoja tu kati ya 11.

Palace imeambulia pointi 26 tu kati ya mechi 36 zilizopita za Ligi Kuu ya England na iko pointi moja tu juu ya Ukanda wa Kushuka Daraja.

Kocha wazamani wa timu ya taifa ya England Sam Allardyce ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kuchukua mikoba ya kocha huyo.

"Kibinafsi nilikuwa na hisia nzuri kuhusu klabu hii ya soka na nina huzuni kubwa muda wangu pale umemalizika, “alisema Pardew, ambaye aliichezea zaidi ya mechi 100 Palace wakati akiwa mchezaji kati ya mwaka 1987 na 1991 na kuiongoza timu hiyo kucheza fainali ya Kombe la FA msimu uliopita, alisema katika taarifa hiyo.

Mwenyekiti wa klabu hiyo Steve Parish aliongeza: "Wakati wa kipindi chake cha kuifundisha timu hiyo, Alan alifanya kazi kwa bidii na alijitahidi kuiimarisha timu hiyo kwa miaka kadhaa.

Hatahivyo, Palace bado haijathibitisha nani atavaa viatu vya kocha huyo katika mchezo wao wa Ligi Kuu ya Enland utakaofanyika Boxing Day.

Pardew aliondoka Newcastle na kutua  Selhurst Park baada ya Neil Warnock kutimuliwa na Palace baada ya timu hiyo ikiwa katika ukanda wa kushuka daraja.

Uteuzi wake ulikuwa maarufu kwa mashabiki wakati Palace ilifanikiwa kukwepoa kushuka daraja kwa kumaliza katika nafasi ya 10, ikiwa ni nafasi yao bora kabisa kuwa kuipata katika kipindi chao cha kucheza Ligu Kuu ya Englnad.

Ina maana alikuwa kocha wa kwanza kabisa katika Ligi Kuu ya England kumaliza katika nusu ya nafasi ya juu baada ya kuwa katika katika ukanda wa kushuka daraja wakati wa Krismas.

No comments:

Post a Comment