Saturday 17 December 2016

Geay, Failuna waing'arisha talent club ya arusha katika Tamasha la michezo la Karatu 2016



Mwandishi Wetu, Karatu
KLABU ya riadha ya Talent ya jijini Arusha jana ilidhihirisha ukali wake baada ya wanariadha wake kushika nafasi za juu katika mbio za kilometa 10  na zile za kilometa tano katika Tamasha la 15 la Michezo na Utamaduni la Karatu.

Mgeni rasmi katika kilele cha tamasha hilo kilichofanyika katika Uwanja wa Mazingira Bora mjini hapa alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye aliyekabidhi zawadi kwa baadhi ya washindi.

Katika mbio za kilometa 10 kwa wanaume, Gabriel Geay wa Talent alishinda kwa kutumia dakika 30:43.93 akifuatiwa na Fabian Joseph wa Arusha dakika 30:48.11 nafasi ya tatu ikikienda kwa Josephat Joshua wa Polisi aliyetumia dakika 30:55. 15.

Mshindi wa nne ni Bazil John aliyetumia dakika 31:12.51 wakati nafasi ya tano ikishikwa na Wilbard Peter dakika 31:40.70 wote kutoka Polisi.

Kwa upande wa wanawake waliokimbia kilometa tano, Failuna Abdi pia wa Klabu ya Talent alishinda akitumia dakika 17:01.49 akifuatiwa na Magdalena Crispin naye wa Talent dakika 17:15.51, nafasi ya tatu ikaenda kwa Jackline Sakilu wa JWTZ dakika 18:10.46.

Watoto waliokimbia kilometa 2.5 wasichana mshindi aliibuka Elizabeth Boniface dakika 9:04.72 akifuatiwa na Rhoda Boniface dakika 9:26.84 wote kutoka Klabu ya Ligwa, huku nafasi ya tatu ikikamatwa na Rozalia Kalole kutoka Mbulumbulu aliyetumia dakika 9:56.55.

Kwa upande wa mbio za Baiskeli kilometa 60 mshindi aliibuka Richard Laizer aliyetumia saa 1:42.13 akifuatiwa na Gerald Didas saa 1:45.58 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Emmanuel Philemon 1:46.27 wote kutoka Arusha.

Baiskeli wasichana mshindi aliibuka Annemarie Griffioen saa 1:10.38 akifuatiwa na Habiba Mathias saa 1:25.40 huku nafasi ya tatu ikinyakuliwa na Lore Desagner saa 1:26.55 wote kutoka Arusha.

Katika soka mabingwa waliibuka Karatu United baada ya kuifunga Viwawa FC kwa mabao 3-0 huku washindi wa tatu wakiwa ni Nyuki FC na nafasi ya nne ikatwaliwa na Laja FC.

Nape Nnauye, ambaye mbali na kuwapongeza waandaaji, aliahidi kuanzia mwakani serikali itaanza kuingiza mkono wake katika kusaidia uandaaji wa tamasha hilo.

Pia, alivitaka vyama mbalimbali vya michezo nchini, kuiga mfano wa Karatu kwa kuandaa matamasha kama hayo ili kuibua na kuendeleza vipaji.

Tamasha hilo ambalo hufanyika kila mwaka, huandaliwa na Filbert Bayi Foundation (FBF), na kudhaminiwa na Olympic Solidarity (OS), kupitia Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC).

No comments:

Post a Comment