Saturday 20 August 2016

Kocha Mourinho ammwagia sifa kiungo mpya wa Man United Pogba wakati Man United ikishinda 2-0



Beki wa Southampton Mreno Jose Fonte (kushoto) akiwania mpira na kiungo mpya wa Manchester United, Mfaransa Paul Pogba wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Old Trafford jijini Manchester,kaskazini ya England.

LONDON, England
KOCHA wa Manchester United Jose Mourinho amempongeza kiungo wake mpya Paul Pogba baada ya mchezaji huyo ghali zaidi duniani kwa mara ya kwanza kuanza katika kikosi cha kwanza wakati wakishinda 2-0 dhidi ya Southampton.

Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa ada ya pauni milioni 89 akitokea Juventus alicheza dakika zote 90, ikiwa ni siku 1,616 baada ya kuichezea timu hiyo mara mwisho.

Alitoa pasi zaidi (71), aligusa mpira (103), alipiga mashuti (4) na alikabiliana na adui (20) zaidi ya mchezaji mwigine yeyote wa Man United.

Mourinho alisema mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa ameonesha kiwango cha hali ya juu.

Zlatan Ibrahimovic alifunga mabao yote mawili kwa Man United, na kufikishamabao matatu katika Ligi Kuu katika mechi mbili. Pia mchezaji huyoa lifunga katika mchezo wa Ngao ya Hisani.

Baada ya mchezo huo, Mourinho aliulizwa kuhusu Pogba, kiungo mwenye umri wa miaka 23 aliyeondoka United kwa pauni milioni 1.5 mwaka 2012 na kwenda Juventus, kabla hajarudi tena katika kipindi hiki cha majira ya joto.

Kwa mara ya kwanza aligusa mpira tangu alipoichezea klabu hiyo wakati waliposhinda mabao 5-0 dhidi ya Wolves Machi mwaka 2012 ilishuhudia akifanya kweli.


Kiungo Mfaransa wa Man United Paul Pogba (kulia) akiwa na mwamuzi Anthony Taylor wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Southampton kwenye Uwanja wa Old Trafford jana.
Mourinho alisema: "Inaonesha uwezo binafsi wa mchezaji. Mchezo wake wa kwanza na alipogusa kwa mara ya kwanza mpira na kuongoza mashambulizi ya kushtua na mipira ya adhabu na kuathiri uchezaji wa wapinzani.

Pogba, ambaye mchezo wake wa mwisho ulikuwa ni ule wa Ufaransa katika fainali ya Euro 2016 walipofungwa na Ureno, alikimbia sawa na kilometa 11.2, ikiwa ni mchezaji watatu aliyekimbia zaidi ya mchezaji mwingine.

"Alicheza dakika 30 zaidi, anaweza kucheza muda wa nyongeza bila tatizo, aliongeza Mourinho.

Pogba alisema: "Ni hisia kubwa. Nilitulia. Nimekuja hapa kushinda, hicho ndicho ambacho nilikuwa nakihitaji. Ni klabu kubwa.

No comments:

Post a Comment