Thursday 15 November 2018

DStv yatangaza neema kwa wateja wake msimu huu wa sikukuu!


Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania Alpha Mria akizungumza jijini Dar es Salaam leo.
 
KATIKA msimu huu wa sikukuu ambapo watu wengi hujumuika na familia zao kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka, MultiChoice Tanzania imetangaza ofa kabambe kwa wateja wake na wale wanaojiunga na huduma za DStv kupitia kampeni yake maalum ijulikanayo kama ‘Ni Muda wa Kukiwasha na DStv’.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania Alpha Mria amesema wateja wa DStv sasa watapata burudani zaidi za kusisimua kupitia Soka, Filamu, Tamthilia, Katuni na vipindi mbali mbali vya watoto vitakavyoileta familia pamoja na kuimarisha upendo.
Msanii wa kujitegemea, Omary Mkali akitumbuiza wakati wa hafla ya Mult-choice leo.

Kwa mujibu wa Alpha, zaidi ya maudhui hayo yote yaliyotajwa hapo juu; Katika kunogesha sikukuu, maudhui mapya yatayoongezwa ndani ya DStv. 

Maudhui hayo ni pamoja na tamthilia ya Kapuni ambayo inaingia msimu wake wa pili katika chaneli ya Maisha Magic Bongo (MMB), Chaneli maalum (EA Movies) yenye mkusanyiko wa filamu bora za Afrika Mashariki, na pia sinema maalum za watoto katika chaneli ya Mnet inayojulikana kama Mnet ANIMANIA pamoja na vipindi mbalimbali vinavyohusiana na msimu huu wa sikukuu. 

Aidha, Alpha alisisitiza kuwa, Kipindi hiki cha sikukuu kupitia chaneli ya Maisha Magic Bongo (MMB) itawaletea wateja maudhui mapya na ya kusisimua zaidi, hivyo kuwasihi watanzania wakae tayari kupokea kitu kipya kutoka MMB tarehe 14 Disemba 2018.
Mkuu wa Mauzo wa kampuni hiyo Salum Salum akizungumza leo.
 Amesema DStv imekuwa mara kwa mara ikiwatunuku wateja wake waliopo na wapya zawadi na ofa kabambe huku wakiendelea kupata burudani ya uhakika muda wote. “Mwaka huu kama kawaida umekuwa mwaka wa neema kwa wateja kwani tumekuwa na mfululizo wa zawadi kwa wateja wetu”

Kwa wateja wapya wanaojiunga na DStv msimu huu watapata ofa maalum ya kuunganishwa kwa shilingi 79,000 pamoja na zawadi maalum ya kifurushi cha mwezi cha Bomba bila malipo ya ziada. Ofa hii itaendelea kwa muda wa miezi miwili kuanzia tarehe 15 Novemba 2018 na ni kwa nchi nzima.
Malkia wa Mipasho Afrika Mashariki, Khadija Omary Kopa.
 Akifafanua kuhusu ofa hiyo, Mkuu wa Mauzo wa kampuni hiyo Salum Salum, amesema kuwa ofa hii ni zawadi ya kufunga mwaka kwa wateja wapya wa DStv kwani katika kipindi cha miezi miwili wataweza kuunganishwa na DStv kwa gharama ya shilingi 79,000 tu na zaidi ya hapo kupewa kifurushi cha Bomba cha mwezi mmoja bila malipo ya ziada.

“Mbali na kuongezwa kwa chaneli na maudhui kedekede kwa wateja walipo wa DStv, pia kwa wale ambao bado hawajajiunga hatujawasahau, sasa tunawapa ofa hiii kabambe ya kujiunga kwa gharama nafuu na zaidi ya hapo wapate kifurushi cha mwezi mmoja bila malipo. Hii ni zawadi yetu ya sikukuu kwa wateja wetu” alisema Salum Salum.

Johnson Mshana na Shumbana wakati wa hafla hiyo leo.
Amesisitiza kuwa ofa hii ni kwa nchi nzima na tayari wameshajipanga na mawakala wote kuhakikisha kuwa ofa hii inapatikana nchi nzima. “Mtu yeyote asiwe na wasiwasi wa jinsi ya kuunganishwa kwa ofa hii. Tunao mawakala wetu wa usambazaji na ufundi nchi nzima, hivyo hata walio maeneo ya vijijini huduma hii watapata.

Wakati huohuo, DStv leo imewakabidhi waandishi wa habari zawadi za ving'amuzi na dishi na kuahidi kuwafungia vifaa hivyo baada ya kujibu maswali vizuri kuhusu 'Ni Muda wa Kukiwasha na DStv’.


No comments:

Post a Comment