Tuesday 15 January 2019

DStv kuonesha Mubashara Michuano ya SportPesa 2019


Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice-Tanzania, Jacqueline Woiso akizungumza na waandishi wa habari wa wakati wa kutangazwa rasmi kwa ushirika kati ya SportPesa na SuperSport ambapo SuperSport kupitia DStv itarusha mubashara michuano hiyo itakayoanza wiki ijayo hapa jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Uendeshaji na Udhibiti wa SportPesa Tanzania Tarimba Abas.

Na Mwandishi Wetu
KING’AMUZI cha DStv ndicho pekee kitaonesha mubashara mashindano ya tatu ya SportPesa yatakayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Januari 22 hadi 27 na kushindanisha timu za Tanzania na Kenya ili kumpata mshindi atakayecheza na Everton, imeelezwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice-Tanzania, Jacqueline Woiso alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa mashindano ya kombe hilo yataoneshwa na DStv kupitia Super Sports, ambayo ndio iliyopata udhini ya kuonesha mashindano hayo kama mshirika rasmi.

Mkurugenzi wa Uendeshaji na Udhibiti wa SportsPesa Tarimba Abas (Katikati) akizungumza wakati wa kutangazwa rasmi kwa ushirika kati ya SportPesa na SuperSport ambapo SuperSport kupitia DStv itarusha mubashara michuano hiyo itakayoanza wiki ijayo hapa jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice TanzaniaJacqueline Woiso na Mkuu wa Uendeshaji Baraka Shelukindo (kushoto)

Mbali na vigogo vya soka Tanzania vya Simba na Yanga, timu zingine zitakazoshiriki katika mashindano hayo ni pamoja na Mbao FC pamoja na Singida United za Tanzania wakati zile za Kenya ni Gor Mahia, AFC Leopard, Bandari na Kariobangi.

Gor Mahia ndio washindi wa kihistoria baada ya kulitwaa taji hilo mara mbili na kufanikiwa kucheza mara mbili dhidi ya Everton inayoshiriki Ligi Kuu ya England.

Michuano hiyo itakuwa na mvuto wa aina yake kwani mbali na ukubwa, umaarufu na utani wa timu shiriki, pia kila timu itataka kutwaa kombe hili na hatimaye kupata fursa ya kucheza na moja ya timu maarufu ya soka nchini Uingereza – Everton FC.

Mkurugenzi wa Uendeshaji na Udhibiti wa SportsPesa Tarimba Abas (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Uendeshaji wa MultiChoice Tanzania Baraka Shelukindo wakati wa hafla ya kutangazwa rasmi kwa ushirika kati ya SportPesa na SuperSport ambapo SuperSport kupitia DStv itarusha mubashara michuano hiyo itakayoanza wiki ijayo hapa jijini Dar es Salaam.

Woiso alisema  jana kuwa SuperSport kupitia DStv itarusha mubashara mashindano hayo yatakayoanza wiki ijayo jijini Dar es Salaam.

 “Tunafurahi kuujulisha umma wa watanzania kuwa hamu yao ya kushuhudia michuano hii mubashara kupitia DStv sasa imepatiwa jibu, sasa watashuhudia burudani hii ya aina yake tena kuanzia kifurushi cha chini kabisa cha Bomba,” alisema Jacqueline.

 “Michezo yote itaonekana kupitia DStv SuperSport 9, ambayo inapatikana katika vifurushi vyote. Tumeamua kufanya hivyo ili kuwapa watanzania fursa ya kushuhudia mashindano haya ambayo yanazidi kujipatia umaarufu kila uchao”.

Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania Jacqueline Woiso akimkabidhi mpira Mkurugenzi wa Uendeshaji na Udhibiti wa SportsPesa Tarimba Abas muda mfupi baada ya kutangaza rasmi ushirika kati ya SportPesa na SuperSport ambapo SuperSport kupitia DStv itarusha mubashara michuano hiyo itakayoanza wiki ijayo hapa jijini Dar es Salaam.

Naye Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa Tanzania, Tarimba Abbas amesema “Tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo miaka mitatu iliyopita, mashindano haya yamekua moja ya mashindano makubwa na yanayopendwa sana Afrika Mashariki yote.

Hili ni jambo kubwa sana kwani wachezaji wetu wataweza kuonesha vipaji na viwango vyao na hivyo kuwatangaza kote duniani. Natoa rai kwa timu zinazoshiriki kuhakikisha zinaonesha viwango vya juu  kabisa kwani huu ni ulingo muhimu wa kuonesha uwezo na ujuzi wao wa soka kwa timu husika lakini pia na kwa wachezaji,” alisema Tarimba.

 Mshindi wa Kombe la SportPesa 2019 atajishindia dola za Marekani 30,000 pamoja na kucheza dhidi ya Everton, moja ya timu maarufu kabisa za soka Uingereza wakati mshindi wa pili atapata dola za Marekani 10,000 wakati mshindi wa tatu atapata dola 7,500 na mshindi wa nne dola 5,000. Timu zote zitakazo tolewa robo fainali zitapata dola 2,500 kila moja.

Michuano ya Kombe la SportPesa ilianza rasmi mwaka 2017 katika michuano iliyofanyika hapa Tanzania, ambapo mshindi – Gor Mahia alicheza na Everton hapa hapa Tanzania. Msimu wa pili wa mashindano hayo yalifanyika huko Nakuru Kenya mwaka jana, mshindi kwa mara ya pili Gor Mahia alikwenda kucheza na Everton huko Liverpool Uingereza mwezi Novemba.

No comments:

Post a Comment