Sunday, 14 February 2016

Van Gaal apokea kichapo England sasa akimbilia Ligi ya Ulaya




LONDON, England
LOUIS van Gaal alikiri kuwa kufuzu kucheza kwa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya itakuwa “ngumu sana” baada ya jana kupokea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Sunderland iliyopo katika nafasi ya pili kutoka mkiani na kuongeza presha kwa kocha Manchester United.

Bao la kujifunga la dakika za mwisho kutoka kwa kipa David de Gea katika mchezo uliofanytika kwenye Uwanja wa Mwangaza kuliifanya Man United kufungwa kwa mara ya kwanza na Wearside katika kipindi cha miaka 19.

Kipigo hicho kimewaacha mabingwa hao mara 20 wa Ligi Kuu ya England kuwa pointi sita nyuma ya timu zinazoshika nafasi nne za kwanza zikiwa zimebaki mechi 12 kabla ya liugi kumalizika baada ya nahodha Wayne Rooney kuwa  "hayakuwa matokeo mazuri kabisa ".

Bao la 10 katika msimu la Anthony Martial kuliifanya Man United kusawazisha kabla ya mapumziko, likifuta lile la kuongoza la wapinzani wao lililowekwa kimiani na Wahbi Khazri, lakini Sunderland iliibuka na ushindi katika mchezo huo.

Ushindi huo umezidi kumuweka matatani Van Gaal, huku tetesi zikizagaa kuwa kocha wazamani wa Chelsea Chelsea Jose Mourinho anajiandaa kuchukua mikoba ya Mholanzi huyo mwishoni mwa msimu.

Van Gaal alisema kuwa kumaliza nafasi yanne ni “mahitaji madogo” kwao kwa klabu hiyo ya Man United.

"Ikiwa Wayne alisema itakuwa vigumu kwetu kumaliza katika nafasi nne za juu, baadae nakubalina naye. Itakuwa vigumu sana kutokana na nafasi yenyewe. Bado inawezekana lakini ni ngumu kweli.

"Tulitakiwa kushinda mchezo huu. Tunataka kuwa katika nafasi nne za mwanzo na sasa ni vigumu sana kuwa katika nafasi hiyo. Lakini hilo ndilo lengo letu, hiyo ni nafasi ya chini tunayohitaji kwa klabu kama hii. Huwezi kulifumbia macho hilo.”

United inaweza pia kufuzu kwa Ligi Kuu kwa kushinda Ligi ya Ulaya.
Timu hiyo itaifuata timu ya Denmark ya FC Midtjylland katika hatua ya 32 ya mashindano hayo Alhamisi na Van Gaal aliongeza: "Unaweza kusema ndio. Hiyo ni njia nyingine ya kufuzu. Lakini kuna baadhi ya vikosi vizuri sana vimeachwa katika mashindano hayo.”
 
Ronaldo azidi kumbeba Zidane Real Madrid 
 
MADRID, Hispania
KOCHA wa Real Madrid Zinedine Zidane ameendelea kumsimu mshambuliaji wake Cristiano Ronaldo baada ya Mredno huyo kufunga mabao mawili wakati kikosi chake kikiibuka na ushndi wa mabao 4-2 katika mchezo wa La Liga dhidi ya Athletic Bilbao.

Mabao hayo mawili ya Ronaldo yamemfanya kufunga bao moja zaidi ya mfungaji anayeongoza katika La Liga Luis Suarez baada ya kufunga mabao 21 katika mechi 32 alizocheza katika mashindano yote msimu huu.

Hatahivyo, mchezaji huy bora mara tatu wa dunia bado amekosolewa kwa kushindwa kuonesha makali yake ya kufunga mabao katika mechi kubwa za Real Madrid ugeni msimu huu.

"Vyombo vya habari viko hapa kwa ajili ya kuangalia kama Ronaldo anacheza vizuri au vibaya, lakini leo ameonesha mchezo mzuri na uwezo wa kufunga, “alisema Zidane.

"Kwangu mimi Cristiano ni mtu muhimu sana katika nafasi ya wingi. Wakati alipobadilisha mchezo hasa anapokuwa akikabiliana na mchezaji mmoja mmoja.

"Nia ni kucheza na Cristiano zaidi katika ushambuliaji wa pembeni…”

Ushindi huo umemfanya Zidane kuwa na mwanzo mzuri kama kocha wa Real Madrid tangu kuchukua nafasi ya Rafael Benitez mwizi uliopita na kutoka sare katika mechi sita za mwanzo.

Hatahivyo, Mfaransa huyo anakabiliwa na mtihani mkubwa hadi sasa wakati Real Madrid itakaporejea katika michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya ugenini dhidi ya Roma Jumatano.

Zaza aizamisha Napoli wakati Juventus ikishika usukani  Italia

ROME, Italia

MCHEZAJI tegemeo la Italia kwa michuano ya fainali za Mataifa ya Ulaya, Euro 2016, Simone Zaza alifunga bao safi katika dakika za mwisho wakati mabingwa Juventus wakiwa pointi moja mbele kileleni mwa Serie A ilipoibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Napoli Jumamosi.

Napoli, hicho ni kipigo chake cha tatu katika kampeni zake za kuwani ubingwa, ilisafiri kaskazini kwa ajili ya michezo miwili dhidi ya mabingwa hao kwa mara ya kwanza tangu katika kampeni za mwaka 2009-2010.

Kwa ushindi huo, Juventus sasa inaongoza katika msimamo wa ligi pamoja na Napoli, ambayo ina saka taji la kwanza tangu mwaka 1990 wakati Diego Maradona alipoiwezesha klabu hiyo ya kusini kutwaa taji lake la pili, sasa ni ya pili na inatofauti ya pointi moja.

Kocha Napoli Sarri wote walikiri kuwa safu ya ulinzi ya Juve ndio ilikuwa chanzo cha wao kufungwa: "Tulikuwa na bahati katika mita 20 mwisho.”

"Miezi nane iliyopita walikuwa pointi 24 nyuma yetu, sasa kama tumelingana.”

Chelsea yaikung'uta Newcastle mabao 5-1




LONDON, England
KLABU ya Chelsea jana ilipata ushindi wa kwanza wa nyumbani wa  Ligi Kuu ya England chini ya kocha wa muda, Guus Hiddink kwa ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya timu inayochechemea ya Newcastle.
Kikosi cha Hiddink kilichezea nyumbani mechi zake zote nne kwenye Uwanja wa Stamford Bridge tangu Mholanzi huyo achukue nafasi kutoka kwa mwenzake aliyetimuliwa Jose Mourinho kama kocha wa muda tangu Desemba.
Lakini Diego Costa ndiye aliyekuwa wa kwanza kuifungia Chelsea kwa bao la mapema kabla Pedro hajaongeza huku Willian na Bertrand Traore wakifunga na kuiwezesha timu hiyo kubuka na ushindi.
Mkosi katika mchezo huo uliibukia baada ya nahodha wa Blues John Terry kutoka nje ya uwanja baada ya dakika 37 kufuatia kuumia, kutokana na kugongana na Aleksandar Mitrovic.
Terry huenda asicheze mchezo wa Jumanne wa hatua ya 16 bora wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya dhidi ya Paris Saint Germain (PSG).
Ushindi huo ni maandalizi mazuri ya Chelsea kwa mchezo huo muhimu dhidi ya PSG, ambapo Pedro alionesha mchezoi mzuri.
Kikosi cha kocha Steve McClaren kilionekana kuwa katika hatari ya kushuka daraja baada ya kuporomoka tena hadi katika nafasi ya tatu mkiani chini ya Norwich kwa tofauti ya mabao.

Saturday, 30 January 2016

yanga yachezea kichapo cha kwanza kutoka kwa Coastal, Simba yaisambaratisha African Sports kwa mabao 4-0



 
Na Waandishi Wetu
MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Yanga jana ilipoteza mchezo wa kwanza katika ligi hiyo baada ya kufungwa mabao 2-0 na Costal Union, huku watani zao Simba wakiondoka na pointi zote tatu dhidi ya African Sports kwa ushindi wa mabao 4-0.

Ushindi huo, unaifanya Simba SC ifikishe pointi 36 baada ya kucheza mechi 16, sasa ikizidiwa pointi tatu tu na Yanga, wanaoongoza kwa pointi 39 sawa na Azam FC ambayo jana haikucheza bambaykila mmoja.aada ya kuwa nchini Zambia kucheza `Bonanza'.
 
Simba iliyocheza kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ilipata bao lake la kwanza dakika ya 14 kupitia kwa mshambuliaji Mganda, Hamisi Kiiza aliyefumua shuti kali kwa mguu wa kushoto baada ya pasi ya beki Hassan Kessy.

Kessy mwenyewe akafunga dakika ya 30 kuipatia Simba SC bao la pili kwa shuti la mguu wa kulia akimalizia pasi ya mshambuliaji Ibrahim Hajib na kumchambua vizuri kipa Zakaria Mwaluko.

Kiiza akamlamba chenga kipa Mwaluko baada ya kupata pasi ya kiungo Mwinyi Kazimoto kuifungia Simba SC bao la tatu dakika ya 42.

Hajji Ugando akaifungia Simba SC bao la nne dakika ya 75 baada ya kupokea nzuri ya kiungo aliyekuwa katika kiwango kizuri.

Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Vincent Angban, Hassan Kessy, Abdi Banda, Juuko Murshid, Hassan Isihaka, Justice Majabvi, Mwinyi Kazimoto/Mussa Mgosi dk86, Jonas  Mkude, Haji Ugando/Said Ndemla dk76, Ibrahim Hajib na Hamisi Kizza/Brian Majwega dk67. 

African Sports; Zakaria Mwaluko, Mwaita Gereza, Halfan Twenye, Juma Shemvuni, Rahim Juma, Mussa Chambega/Hussein Amir dk51, Ally Ramadhani, Pera Ramadhani, Hamad Mbumba, Rajab Isihaka na James Mendy/Mohammed Issa dk56.

KWA UPANDE WA YANGA:

Yanga imefungwa mabao 2-0 na Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na matokeo hayo yanawafanya wabaki na pointi zao 39 baada ya kucheza mechi 16, sawa na Azam FC iliyocheza mechi 15.

Coastal Union walipata bao lao la kwanza dakika ya 27 kupitia kwa beki wa zamani wa Simba,   Miraj Adam aliyefunga kwa shuti la mpira wa adhabu lililomparaza mikononi kipa Deo Munishi ‘Dida’ kabla ya kutinga nyavuni.

Refa Andrew Shamba wa Pwani aliwapa nafasi ya kupiga faulo Coastal Union, baada Miraj Adam mwenyewe kuangushwa na beki wa Yanga, Kelvin Yondan nje kidogo ya boksi.

Mshambuliaji chipukizi, Juma Mahadhi aliifungia bao la pili Coastal Union dakika ya 62 baada ya pasi nzuri ya Hamad Juma.

Bao hilo liliwavunja nguvu kabisa wachezaji wa Yanga SC na kujikuta wanacheza bila malengo. Refa Andrew Shamba alimtoa kwa kadi nyekundu beki wa Yanga, Kevin Yondan dakika ya 100.
Awali, dakika ya 97 Shamba alijichanganya kwa kumuonyesha kadi nyekundu Said Jeilan badala ya njano.

Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Deogratias Munishi, Juma Abdul, Oscar Joshua, Kelvin Yondan, Vincent Bossou, Mbuyu Twite, Simon Msuva, Thabani Kamusoko, Amissi Tambwe/Paul Nonga dk76, Donald Ngoma na Deus Kaseke/Issoufou Boubacar dk80.

Coastal Union; Fikirini Bakari, Hamad Juma, Adeyoum Ahmed, Said Jeilan, Miraji Adam, Sabo Youssouf, Juma Mahadhi/Omar Wayne dk86, Ayoub Yahya/Mtenge Juma dk97, Chidiebele Abasarim, Ally Ahmed  na Ismail Mohammed.


CONGO DR YAWAFUNGISHA VIRAGO WENYEJI RWANDA KWA KUIFUNGA 2-1 KATIKA MUDA WA NYONGEZA



KIGALI, Rwanda
JAMHURI ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ilihitaji muda wa ziada kuwaondosha wenyeji Rwanda katika mashindan ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani (Chan), baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa robo fainali jijini hapa.

Doxa Gikanji aliipatia Congo bao la kuongoza dakika 10 tangu kuanza kwa mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Amohoro.

Hatahivyo, wenyeji walisawazisha dakika 12 baada ya mapumziko kwa bao lililowekwa kimiani na Ernest Sugira.

Padou Bompunga aliifungia Congo bao la ushindi katika muda wa nyongez na hiyo ikiwa na maana kuwa washindi hao sasa watakutana ama na Zambia au Guinea katika nusu fainali itakayopigwa Jumatano.

Congo, ambayo iliwahi kutwaa taji hilo mwaka 2009, ilipata uongozi wa mchezo wakati Rwanda iliposhindwa kuokoa vizuri mpira na mpira huo kuangukia kwa Gikanji aliyekuwa nje ya eneo la hatari na kupiga shuti kali na kumuacha kipa wa Rwanda Eric Ndayishimiye akishindwa kuokoa shuti hilo.

Dakika tisa baadae, huku Chui hai wa Congo wakiwa wametawala, Jonathan Bolingi alipiga shuti lililogonga mwamba.

Bao la kusawazisha la Rwanda la kipindi cha pili lilipatikana kutoka kwa Sugira likiwa ni bao lake la tatu.

Mchezaji huyo alifunga bao hilo baada ya kufanikiwa kuwa nyuma ya mabeki wa Congo, na kupiga shuti lililompita kipa Ley Matampi.

Muda mfupi baadae mchezaji huyo nusura afunge baada ya kuitoka beki ya Congo na Matampi akiwa yeye na kipa, alipiga juu ya wavu wa goli.

Timu zote zilishambuliana kwa zamu kabla ya filimbi ya mwisho, lakini hadi dakika 90 za kawaida za mchezo zinamalizika, timu hizo zilikuwa sare ya bao 1-1.

Wakati muda ukiendelea kuyoyoma watu wakitarajia timu hizo zitapigiana penalty kumpata mshindi, Bompunga alipiga mpira wa kichwa cha nyuma na mpira kumpita Ndayishimiye.

Serena Williams atolewa nishai na kibonde Australian Open



MELBOURNE, Australia
MCHEZAJI Angelique Kerber huku akishangiliwa na mashabiki kwenye Uwanja wa Rod Laver Arena leo Jumamosi usiku ikiwa ni zaidi ya saa mbili alikiangusha kigogo Serena Williams na kutwaa taji la micbuano ya tenisi ya Australian Open.

Kerber alimchapa Serena ambaye ni bingwa namba moja kwa ubora katika mchezo huo duniani kwa upande wa wanawake kwa 6-4, 3-6, 6-3. Ni taji la kwanza kubwa kwa Kerber, na ni la kwanza kwa mchezaji wa Ujerumani katika karne hii.

Kerber, ambaye ana umri wa miaka 28 na ni mwaka wake wa 14 katika katika mchezo huo, alikuwa akicheza fainali yake ya kwanza ya mashindano makubwa, ambapo alianza mmchezo huo kwa kuokoa mpira uliopigwa na bingwa huyo mara 21, kabla hajafanya matokeo ya kuongoza kwa 2-0.

Bingwa huyo alijikuta mipira mingi aliyoipiga iliishia kwa Kerber, na Kerber alifanya kweli na kuendelea kumsambaratisha mpizani wake.

Williams lionesha kuzinduka katika seti ya pili baada ya kucheza vizuri na kumuwezesha kufikia hatua hiyo bila ya kupoteza seti hiyo. Mchezo huo uliendelea na mshindi kuamriwa katika seti ya tatu.

Mashabiki walipagawa baada ya Kerber akipomsambaratisha Williams katika mchezo wa kwanza.
Ilikuwa ni kawaida kwa mashabiki uwanjani hapo kulipuka kwa furaha kwa kumshangilia Kerber. 

Mashabiki wa mchezo wa tenisi wa Australia mi kawaida yao kumshangilia mchezaji asiyepewa nafasi ya kushinda, lakini Williams alisema kuwa huo ni uwanja anbo amekuwa akihisi kupendwa sana.

Williams aliwaambia waandishi wa habari Alhamisi kuwa, ilikuwa miujiza kucheza fainali hapa. Baada ya kushinda hii na mataji mengine mawli makubwa  mwaka jana. Alitarajia kuanza taratibu mashindano hayo. Alikuwa nje ya uwanja kwa miezi minne akiuguza maumivu ya kufungwa katika nusu fainali ya mashindano ya U.S. Open. Alitarajia kuanza taratibu, alisema.