Friday, 23 February 2018

Mechi Kali za Premier League Wikiendi hii


WIKIEND hii kwenye michuano ya Premier League, Liverpool inarudi uwanjani siku 10 baada ya ushindi mzito wa 5-0 walioupata dhidi ya Porto kwenye Ligi ya Mabingwa UEFA, Jumamosi hii kwenye EPL wanawakaribisha Westham United Anfield wakiwa na matumaini makubwa ya kupata matokeo, Je watafanikiwa?

Angalia mechi hii MUBASHARA kwenye DStv Bomba kwa sh.19,000 tu, mechi itachezwa saa 12 jioni ,Supersport 10.

Mechi nyingine zitakazopigwa wikiendi hii kwenye Premier League ni:

        Leicester City dhidi Stoke City saa 9 alasiri kwenye Supersport 3

        Watford vs Everton saa 2 usiku kwenye Supersport 3

        Burnely vs Southampton saa 12 jioni Supersport 5

        Na AFC Bournemouth itacheza dhidi ya Newcastle United saa 12 jioni a kurushwa LIVE kwenye Supersport 10 iliyopo kwenye kifurushi Bomba kw ash.19,000 tu!

Jumapili ndio balaa lenyewe pale Manchester United ambao kwasasa wanashika nafasi ya 2 kwenye msimamo wa EPL wakiwa na pointi 56 wanawakaribisha Chelsea ambao wapo nafasi ya 4 wakiwa na utofauti wa pointi 3 tu! Je, Man Utd atashinda au Chelsea itafunga pengo?

Usikose mechi hii, Jumapili saa 10 jioni kwenye Supersport 3 ya kifurushi DStv Compact kwa sh.69, 000 tu!

Je hujajiunga na DStv?  wahi sasa Ofa ya THE PUNGUZO, burudika na miezi miwili bure kwa kununua Dekoda pamoja na Dish kwa sh.79, 000 tu!

Kujiunga piga 0659 070707, THE PUNGUZO na DStv!!


Zabuni 163 za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya biashara Termina 3 zafunguliwa leo

Ofisa Manunuzi na Ugavi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bi. Margareth Mushi akifungua boksi lililohifadhia zabuni za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya biashara katika jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.   

 

Boksi lililokuwa limehifadhi nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya biashara kwenye Jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere likiwa tupu baada ya nyaraka hizo kuondolewa tayari kwa ufunguzi leo.

Nyaraka za zabuni za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na kuwekeza katika maeneo ya biashara kwenye Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere zikiwasili  Jengo la Kwanza la abiria (TB1) ili ziingizwe kwenye ukumbi na kufunguliwa.


Maboksi ya zabuni mbalimbali za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na uwekezaji katika maeneo ya biashara kwenye Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere yakishushwa kwenye gari kabla ya kuingizwa katika ukumbi wa mikutano wa Transit uliopo jengo la Kwanza la abiria (TB1).


Wananchi walionunua zabuni za kuwekeza katika ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya biashara kwenye jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere leo wakifuatilia kwa makini wakati wa ufunguaji wa zabuni hizo katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Kwanza la abiria (TB1).

Ofisa kutoka kampuni inayotoa huduma ya mizigo ndani ya viwanja vya ndege ya Nas Airco, Bw. David Ngarapi (anayetazama kamera) akifuatilia zoezi la ufunguaji wa zabuni za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya kuwekeza katika maeneo ya biashara kwenye Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere zilizofunguliwa leo kwenye ukumbi wa Jengo la Kwanza la abiria (TB1).

Kaimu Mkuu wa Idara ya Manunuzi na Ugavi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Godfrey Kanyama (kushoto) akisikiliza swali kutoka kwa Mama Open Kitchen (Mama Ntilie wa Kishua), wakati wa ufunguzi wa zabuni za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na uwekezaji kwenye maeneo ya biashara kwenye Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.

 

Tuesday, 20 February 2018

Marubani wa Kenya Waliotekwa Warejea


NAIROBI, Kenya

MARUBANI wawili wa Kenya ambao walikuwa wakishikiliwa na kundi la magaidi Sudan Kusini kwa zaidi ya mwezi mmoja wamerejea nyumbani.

Walitua kwenye Kiwanja cha Ndege Nairobi kabla hawajakutana na ndugu zao.

Rubani Njoki akikutana tena na mtoto wake wakike mwenye umri wa miaka 12, Lucy Muthoni.

Magaidi hao waliwakamata wawili hao mapema mwezi uliopita wakati ndege ilipoanguka katika mkoa wa  Upper Nil, ikiripotiwa kuuwa mwanamke mmoja na baadhi ya mifugo.

Marubani hao wawili waliachiwa juzi kufuatia mazungumzo mazito ya makubaliano yaliyowashirikisha viongozi wa serikali ya Sudan Kusini na wenzao wa Kenya.


Serikali Yaipiga Stop RT Kuongeza Tozo za Mbio

 

Sunday, 18 February 2018

Ndege Yaanguka na Kuuwa Abiria 66 Iran


TEHRAN, Iran
WATU 66 wamekufa baada ya ndege ya abiria kuanguka Iran, maofisa wa ndege hiyo wamesema.
Ndege hiyo ya Shirika la Ndege la Aseman, ilikuwa ikifanya safari yake kutoka Tehran kwenda katika jiji la kusini-magharibi la Yasuj, ilianguka katika milima ya Zagros.
Shirika la Misaada la Mwezi Mwekundi liituma timu yake ya waokoaji kwenda karibu na eneo la tukio karibu na jiji la Semirom katika jimbo la Isfahan.
 Ndege namba EP 3704 iliondoka Tehran saa 2:00 asubuhi kwa saa za hapa na saa chache baadae ilipotea katika rada.
Ndege hiyo ilianguka katika Mlima wa Dena, ikiwa ni kilometa 22 kutoka Yasuj, taarifa ya chaneli ya Irinn iliripoti.
 Ndege hiyo imetengenezwa Ufaransa yenye injili mbili za ATR 72-500.
Ndege hiyo ilikuwa na jumla ya abiria 60, wawili walinzi wa usalama, wawili wafanyakazi wa ndege na rubani pamoja na msaidizi wake.
"Baada ya kuitafuta katika eneo hilo, bahati mbaya tulitaarifiwa kuwa ndege hiyo imedondoka. Na kwa bahati mbaya abiria wetu wapendwa wote wamepoteza maisha.”

DStv Media Bonanza Yafanyika kwa Kishindo Dar

Meneja Uendeshaji wa Multichoice-Tanzania, Ronald Shelukindo (kulia) na Mkuu wa kitengo cha Mawasilinao cha kampuni hiyo, Johnson Mshana wakizungumza na wadau mbalimbali waliofika katika hafla ya DStv Media Day Bonanza Gymkana Club jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
WAANDISHI wa Habari kutoka vyombo mbalimbali leo walijumuika pamoja katika DStv Media Bonanza lililofanyika katika viwanja vya Gymkana Club Jijini Dar es Salaam.

Katika Bonanza hilo, timu ya soka inayoundwa na wafanyakazi wa DStv na ile inayopundwa na waandishi wa habari kutoka vyombo mchanganyiko (Taswa FC) ziliumana na kutoa burudani safi kwa watu mbalimbali waliofika hapo.
Johnson Mshana akiwa na wadau.
Katika mchezo huo, timu ya Taswa FC iliibuka na ushindi wa mabao 6-2 dhidi ya wapinzani wao hao, ambao walitamba katika kipindi cha kwanza na kushindwa kuendeleza cheche zao kipindi cha pili.

Katika bonanza hilo lililoanza majira ya saa 6:00 mchana hadi 12:00 jioni, washiriki waliburudika na burudani mbalimbali zikiwemo muziki wa dansi `live’ na burudani nyingine.
Pia walipata vinywaji na msosi huku wakibadilishana mawazo baada ya wengine  kutoonana kwa muda mrefu, ambapo hafla hiyo iliwakutanisha waandishi wa vyombo mbalimbali huku DStv ikiahisi kuendelea kushirikiana nao.



Kikosi cha DStv kabla ya kuanza kwa mchezo dhidi ya Taswa FC.

Vikosi vya DStv (wenye jezi bluu) na Taswa FC (nyeupe) kabla ya kuanza kwa mchezo wao wa kirafki.



Kikosi cha Taswa FC


Mhariri wa gazeti la Dailynews na Sundaynews, Nasongelya Kiyinga akisalimia na mfanyakazi wa DStv, Levina wakati wa hafla hiyo.

Mtangazaji wa SuperSport na mwandishi mkongwe nchini, Aboubakary Liongo akisalimiana na mwandishi wa Mtanzania, Mwani Nyangasa.


Kikundi cha ushangiliaji cha DStv wakati timu yao ilipocheza dhidi ya Taswa FC. Taswa ilishinda 4-2.


Baadhi ya waandishi wakichukua msosi wakati wa bonanza hilo.




Mchezaji wa Taswa FC, Majuto Omary `Bonge' akitafuta njia ya kuwatoka wachezaji wa DStv wakati wa mchezo wa kirafiki wa DStv Media Day Bonanza mapema leo Gymkana Club Jijini Dar es Salaam. Taswa ilishinda 6-2.

Thursday, 15 February 2018

DStv Media Day Bonanza Kufanyika Kesho


Na Mwandishi Wetu
BONANZA kubwa la Waandishi wa Habari lintarajia kufanyika kesho Jumamosi katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, imeelezwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shumbana Walwa wa DStv, bonanza hilo litashirikisha Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini.

Katika bonanza hilo kutakuwa na michezo mbalimbali, ambapo timu ya wafanyakazi wa DStv watatoana jasho na timu ngumu ya soka ya Chama cha Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, Taswa.
Mbali na mchezo huo na mingine, pia kutakuwa na burudani live ya muziki wa dansi, ambapo wageni waalikwa wataburudika kwa muziki huo kabambe.

Pia waandishi pamoja na wadau wengine wa habari, watapata chakula cha mchana pamoja kuhitimisha shughuli hiyo, ambayo hufanyika kila mwaka.

DStv wafungua tawi jipya, watoa ofa kabambe


Na Mwandishi Wetu
MULTCHOICE Tanzania leo Ijumaa itazindua tawi lake jipya katika eneo la bishara la Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo, inasema kuwa hatua hiyo ya kufungua tawi eneo hilo maarufu ni kwa ajili ya kuwasogezea huduma ya DStv wateja wao wa maeneo  mbalimbali wanaofika maeneo hayo kupata huduma zingine.

Katika kusheherekea Msimu huu wa Valentine, DStv hawajakusahau, wanakuletea huduma zao karibu zaidi na kukupa zawadi Kabambe ya Valentine.

Taarifa hiyo imezidi kueleza kuwa, tawi hilo limesheheni huduma zote na wafanyakazi wacheshi na wakarimu wako tayari kabisa kukuhudumia.

Ili kuzidi kuleta msisimko kwenye valentine hii, DStv wanakuletea Ofa maalum kwa wateja wa tawi lao la Mlimani City pekee, fika tawini kuanzia tarehe 13 hadi 18 February upate kununua Dikoda, Dishi na Vifaa vyote  kwa sh.69,000 tu pamoja na miezi miwili buree!!

Ofa hii haishii hapo ndugu yangu, DStv watakupatia Na ufundi buree. Yaani hii ni The Punguzo Valentine Special!

Wahi sasa kwenye ofisi zao mpya zilizopo Mlimani City opposite na zamani Nakumat Supermarket.

Wednesday, 14 February 2018

Maisha Magic Bongo Kufadhili Harusi ya Aina Yake

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania Maharage Chande (katikati) akiwa na maharusi watarajiwa, Solomon Mwaigwisa na Magreth Richard wakati wa kuwatangaza wawili hao kushinda shindano la Harusi ya Ndoto Yako leo asubuhi Jijini Dar es Salaam. 


Na Mwandishi Wetu
WAKAZI wawili wa jijini Dar es Salaam ambao ni wachumba, Solomon Mwaigwisa na Magreth Richard wameibuka washindi wa shindano la Harusi ya Ndoto Yako lililokuwa likiendeshwa na chaneli ya Maisha Magic Bongo Dstv chaneli 160.

Wapenzi hao wameshinda zawadi ya ufadhili wa harusi yao ya kifahari itakayofanyika jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa April mwaka huu.  Pamoja na kushinda Harusi ya Ndoto Yao, wawili hawa pia watapewa zawadi ya fungate kwa hisani ya hoteli ya kitalii ya Voyager Beach iliyopo jijini Mombasa nchini Kenya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice-Tanzania, Maharage Chande.
Washindi hao walitangazwa leo asubuhi katika kilele cha Siku ya Wapendanao katika hafla iliyofanyika makao makuu ya MultiChoice Tanzania jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na washindi hao.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania Maharage Chande amesema channel ya Maisha Magic Bongo imeamua kuwatunuku watazamaji wake zawadi hiyo kupitia kipindi chake maarufu cha Harusi Yetu kinachorushwa na channel hiyo ambacho huonyesha harusi mbalimbali.
Kipindi cha Harusi Yetu kilianza kuruka Novemba 2016, ambapo msimu wa pili wa kipindi hicho ulianza mwezi Julai mwaka 2017. Kipindi hicho hurusha harusi mbamlimbali huku kikiangazia walikotoka wanandoa, hatua wanazopitia katika mahusiano yao na hatimaye tukio la kufunga ndoa.

Kuanzia ilipoanza awamu ya pili Maisha Magic Bongo ilianzisha shindano maalum lililojulikana kama Harusi ya Ndoto Yako ambapo washiriki walikuwa wakijibu kuhusiana na kipindi cha harusi yetu ambapo kila wiki kulikuwa na swali moja.

Waandishi wa habari wakifuatilia hafla hiyo.
Hadi kufikia mwisho wa shindano mnamo mwezi Desemba mwaka jana jumla ya washiriki 1,112 walishiriki ambapo 448 waliingia kwenye mchujo wa wawali na hatimaye kubakia wanne ambao waliitwa kwenye usaili maalum uliokuwa na jopo la watahini saba.

Baada ya usaili huu, Solomon mkazi wa Dar es Salaam pamoja na mchumba wake Magreth waliibuka washindi na hivyo kupata zawadi ya kugharimiwa harusi yao itakayofanyika jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 28 mwezi April mwaka huu.
Mfanyakazi wa DSTV, Shumbana. 
Akifafanua kuhusu zawadi hiyo, Maharage alisema zawadi hiyo inamaanisha maharusi hao watarajiwa watagharimiwa kila kitu kuanzia ukumbi, mavazi, chakula, vinywaji, burudani, pamoja na fungate la kukata na shoka katika moja ya hoteli za kitalii Voyager Beach Hotel katika ufukwe wa Mombasa nchini Kenya.

Wakizungumza katika hafla hiyo, Solomon pamoja na mchumba wake Magreth wamesema wamefurahi sana kushinda na kutuzwa ufadhili wa harusi yao. “Sote tunafahamu ni jinsi gani zoezi la harusi linavyokuwa na patashika hususan kwenye suala la gharama.
Maharusi watarajiwa, Solomon na Magreth wakiingia stejini.
“ Hivyo nafurahi sana na ninamshukuru Mungu kwa kutuwezesha kushinda katika shindano la Harusi ya Ndoto Yangu kwani sasa sisi kazi yetu ni kufikiria tu jinsi tutakavyoendesha maisha yetu kwani suala la harusi limekamilika” alisema Solomon, ambaye ni Bwana Harusi mtarajiwa.

Ameipongeza Chaneli ya Maisha Magic Bongo kwa kubuni shindano hilo ambalo lilileta msisimko mkubwa na kwamba anaamini kuwa channel hiyo itaendelea kuimarika kwani kwa sasa imekuwa maarufu sana kwa kuwa ni chaneli inayowafanya watanzania wajivunie vipaji vyao.
Bi Harusi Mtarajiwa, Magreth.
DStv kupitia chaneli yake mahsusi ya maudhui ya Kitanzania ya Maisha Magic Bongo imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa tasnia ya Sanaa inakua na kuifanya iwe moja ya vyanzo muhimu vya mapato kwa wasanii na hatimaye kuchangia katika uchumi wa nchi yetu.

Chanel ya Maisha Magic Bongo ilianzishwa tarehe 1 Octoba 2015, kwa lengo kuu la kuinua na kukuza vipaji na Sanaa hapa Tanzania na pia kuongeza maudhui ya kitanzania kwa wateja wa DStv.
Maharusi watarajiwa wakati wa hafla hiyo.
Kwa kipindi chote hiki Chaneli hii imekua kwa haraka sana ambapo kwa sasa ni miongoni mwa Chaneli zenye watazamaji wengi zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki. Chaneli hii imekuwa kitovu cha maendeleo ya wasanii hapa nchini huku mamia ya wasanii wakipata fursa mbalimbali kutokana na kazi zao kurushwa katika channel hii na pia kupata mafunzo na kipato kupitia Sanaa.

Kwa upande wa tasnia ya filamu na uigizaji, Maisha Magic Bongo imeleta mapinduzi makubwa na miongoni mwa filamu zinazotikisa katika soko kwa sasa ni pamoja na Tamthila ya HUBA,ambayo ilipokelewa vizuri sana na Watanzania, pia kuna filamu na vipindi vingine kama MWANTUMU, HARUSI YETU, KITIMTIM pamoja na tamthilia mpya zilizoanza kuonyeshwa hivi karibuni za SARAFU na KAPUNI ambazo zote zinazidi kuwa maarufu kila uchao.

Wedding Planner wa harusi hiyo.