Wednesday, 18 May 2016

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan Ijumaa kuzindua mfuko wa uchangishaji fedha za kupambana na Ukimwi


Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kupambana na Ukimwi (Tacaids), Dk. Fatma Mrisho akizungumza na waandishi wa habari leo. Kulia ni makamu wa rais wa Geita Gold Mine (GGM), Simon Shayo na Balozi wa Kili Challenge, Mrisho Mpoto.

Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan Ijumaa atakuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kuchangisha fedha kwa ajili ya kupambana na Ukimwi utakaofanyika jijini Dar es Salaam, imeelezwa.

Hafla hiyo imeandaliwa na Mgodi wa  Dhahabu wa Geita (GGM) kwa kushirikiana na Tume ya Kupambana na Ukimwi Tanzania (Tacaids),ambapo mwaka huu wanatarajia kukusanya zaidi ya sh. bilioni 1.
Makamu wa Rais wa GGM, Simon Msuya akzungumza na waandishi wa habari mapema leo. Wengine pichani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tacaids, Dk. Fatma Mrisho na Balozi wa Kili Challenge Mrisho Mpoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tacaids, Fatma Mrisho alisema jana kuwa GGM kwa kushirikiana na Tacaids kila mwaka imekuwa ikichangisha fedha kwa ajili ya kusaidia vituo na taasisi mbalimbali zinazopambana na Ukimwi.

Fedha hizo zitachangishwa kwa utaratibu wa kupanda Mlima Kilimanjaro, ambapo watu mbalimbali wanatarajia kuchangia, ambapo fedha hizo zitasaidia vituo mbalimbali vinavyosaidia waathirika wa Ukimwi.

Balozi wa Kili Challenge, Mrisho Mpoto au Mjomba (kushoto) akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam. Katikti ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tacaids, Dk. Fatma Mrisho na makamu wa rais wa GGM, Simon Shayo.
Alisema vifo vitokanavyo na Ukimwi vimepungua kwa takribani asilimia 40 lakini vinatakiwa kufikia asimilia 100.

Aidha, makamu wa rais wa GGM Simon Shayo alisema kuwa kesho katika hafla hiyo pia wataitumia kuzipa fedha taasisi mbalimbali za umma na zila za binafsi zinazopambana na Ukimwi.

Alisema mwaka jana walikusanya kiasi cha Sh Bilioni 1 na mwaka huu wanatarajia kukusanya fedha zaidi kwa ajili ya kusaidia vikundi au taasisi zinazopambana na Ukimwi.

Alisema GGM itaendelea kushirikiana na serikali katika vita hiyo ya kupambana na ukimwi ili kuhakikisha unapungua na kumalizika kabisa ifikapo mwaka 2030.

Alisema kuwa katika hafla hiyo kesho watatoa fedha zilizokusanywa mwaka jana kwa taasisi mbalimbali.

Balozi wa Kili Challenge Mrisho Mpoto alisema kuwa jana kuwa  jamii bado ina unyanyapaa kwa watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI pamoja na UKIMWI, ambapo hali hiyo inasababisha kuchelewa kukabiliana na janga hilo.

Imeelezwa kuwa tatizo hilo limesababisha waathirika wa tatizo hilo kuwa na woga kwa kuhofia unyanyapaa miongoni mwa jamii, kitu ambacho kinaumiza sana.
 
Alisema kuwa, usiri huo na elimu ndogo ya kukabiliana na ugonjwa huo ikiwemo matumizi sahihi ya kinga na dawa za kupunguza makali yake vimezidi kufanya hali izidi kuwa mbaya.

Alisema atajitahidi kuhakikisha uteuzi wake unakuwa na matokeo chanya katika jamii, hasa vijana ambao ndio waathirika wakubwa wa ugonjwa huo hapa nchini.

Kwa kipindi kirefu sasa Tanzania imeendelea kuwa na watu wengi wanaoishi na Virusi vya Ukimwi pamoja na wagonjwa wa Ukimwi.

Kwa mujibu wa takwimu kutoka Tacaids, inakadiriwa kuwa watu milioni 1.6 nchini wanaishi na VVU na Ukimwi, na kuwaathiri zaidi ya vijana na watoto yatima milioni 1.3.

Bado ipo changamoto miongoni mwa jamii kuhusu elimu ya ugonjwa huo kwa kuwa kuna vituo vichache sana vya taarifa juu ya janga hilo.

GEITA GOLD MINE (GGM) NA TACAIDS WAUNGANA KUPAMBANA NA UKIMWI


 
Rais Mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa akikabidhi mfano wa hundi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa  Tume ya Kupambana na Ukimwi, Dk. Fatma Mrisho. Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa GGM, Terry Mulpeter wakati wa uzinduzi rasmi wa Kili Challange kwa mwaka jana.

KWA Kipindi kirefu sasa Tanzania imeendelea kuwa na watu wengi wanaoishi na Virusi vya UKIMWI pamoja na wagonjwa wa UKIMWI.Kwa mujibu wa takwimu kutoka Tume ya Kupambana na UKIMWI nchini (TACAIDS) inakadiriwa kuwa watu milioni 1.6 nchini wanaishi na VVU na Ukimwi. Ugonjwa huu umewaathiri zaidi vijana na watoto yatima zaidi ya milioni 1.3.

Bado ipo changamoto miongoni mwa jamii kuhusu elimu ya ugonjwa huo kwa kuwa kuna vituo vichache sana vya taarifa juu ya janga hilo.Jamii bado ina unyanyapaa kwa Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI pamoja na UKIMWI.

Hali hii ndiyo inayosababisha tuchelewe kukabiliana na janga hili.Waathirika wa tatizo hili wamekuwa woga kwa hofu ya unyanyapaa miongoni mwa jamii.Usiri huu na elimu ndogo ya kukabiliana na ugonjwa huu ikiwemo matumizi sahihi ya kinga na dawa za kupunguza makali yake vimezidi kufanya hali izidi kuwa mbaya

Katika kukabiliana na changamoto hiyo na kuisaidia serikali kufikia lengo namba tatu la Malengo endelevu ya Maendeleo ya Umoja wa mataifa  ya kuwa na jamii yenye afya bora ifikapo 2030,Mgodi wa Dhahabu wa Geita(GGM) kwa kushirikiana na Tume ya Kupambana na UKIMWI nchini (TACAIDS) umendelea tena kuchangisha fedha ili kupambana na UKIMWI kupitia Kampeni yake ya KILI CHALLENGE.
 
KILI CHALLENGE ni kampeni iliyoanza mwaka 2002 ambayo hufanywa kila mwaka kwa wadau mbalimbali kupanda mlima Kilimanjaro na kuchangisha fedha kwa ajili ya kutunisha mfuko wa mapambano dhidi ya Virusi vya UKIMWI pamoja na UKIMWI.
 
Mwaka 2015 pekee Kampeni hii ilifanikiwa kukusanya takribani shilingi za Kitanzania Bilioni Moja. Fedha hizo zitatolewa kwa wadau mbalimbali wanaojishughulisha na mapambano ya Ukimwi katika uzinduzi wa upandaji Mlima kwa mwaka huu pale Hyatt Hotel, Dar es Salaam Ijumaa tarehe 20 Mei. 

Mgeni rasmi katika Hafla hiyo atakuwa makamu wa Raisi Mhe. Samia Suluhu.

Makamu wa Rais wa miradi endelevu wa Anglogold Ashanti (GGM) Bw. Simon Shayo amesema kuwa Kampeni ya Kili Challenge mwaka huu itakuwa na utofauti mkubwa kwa kuwa inafanyika chini ya Serikali mpya.

Kwa miaka 15 iliyopita tumeshirikiana vizuri na Serikali zote pamoja na wadhamini mbalimbali ambao wamekuwa wakituunga mkono kutuchangia fedha ili kupambana na tatizo hili.
 
Tunaamini kuwa Serikali mpya chini ya Rais  Dkt John Pombe Magufuli ambayo imekuwa ikifanya jitihada nyingi kununua dawa na kuboresha huduma za Afya itatuunga mkono katika Kampeni yetu mwaka huu.Anaeleza Bwana Shayo.

Zaidi ya Asasi 30 zimeweza kunufaika na Mfuko huu katika kipindi cha miaka 15 iliyopita. Baadhi ya asasi hizi ni pamoja na TACAIDS, Benjamin Mkapa Foundation, Geita Hospital na nyinginezo.

Shayo amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kwa wingi kuchangia fedha katika Kampeni hiyo ili kusaidia kupunguza ongezeko la maelfu ya watoto yatima wanaohitaji misaada baada ya wazazi wao kufariki.

Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho amesema, Tukifanikiwa kushiriki kikamilifu katika Kampeni hii tutafanikiwa pia kusaidia wajane wasiokuwa na kipato pamoja na wazee wanaolazimika kuwalea wajukuu walioachwa na watoto ambao walifariki kutokana kwa ugonjwa huo 

Kilimanjaro Challenge imebakia kuwa Asasi pekee inayoleta kwa pamoja serikali na Makampuni binafsi kwa ajili ya mapambano dhidi ya VVU & Ukimwi kwa jamii ya Kitanzania na dunia kwa ujumla ili kuwapa matumaini ya kuhakikisha jamii inabaki bila kuathiriwa na ugonjwa huo katika miaka ijayo.

Mpango huo pia unalenga kuisaidia Serikali kukabiliana na VVU & Ukimwi sambamba na kutoa nafasi kwa watalii wa ndani kuupanda mlima Kilimanjaro.

KUHUSU Kili Challenge:
Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya www.anglogoldashanti.com  na www.geitakilichallenge.com

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:-
Tenga B Tenga Manager, Public Relations & Communications
Email: ttenga@anglogoldashanti.com  Tel: +255 282 160 135 | +255 689 103 619

Kocha Louis van Gaal akiri mashabiki Manchester United walitarajia mafanikio makubwa


Beki wa Manchester United, Chris Smalling (kushoto) akigombea mpira na mshambuliaji wa Bournemouth, Joshua King wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Old Trafford jana. Mchezo huo awali ulipangwa kufanyika Mei 15, lakini uliahirishwa baada ya kutokea kwa tishio la bomu kwenye uwanja huo.

LONDON, England
KOCHA wa Manchester United Louis van Gaal anasema mashabiki wa timu hiyo walitarajia mambo makubwa kutoka katika klabu hiyo ya Old Trafford.

Man United iliifunga Bournemouth jana na kumaliza ya tano katika Ligi Kuu ya England, lakini mabingwa hao mara tatu wa Ulaya wamekosa nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kwa mara ya pili katika misimu miwili.

"Timu yetu iko katika mpito na na kama nilivyosema tangu mwanzo, alisema Van Gaal, ambaye alianza kuifundisha timu hiyo katika kipindi cha majira ya joto ya mwaka 2014.

"Labda nilihitajika kutuma ujumbe mzuri zaidi ya nilivyofanya.

Kocha wazamani wa Uholanzi Van Gaal alisaini mkataba wa miaka mitatu baada ya kuichukua timu hiyo miezi mitatu tangu alipotimuliwa David Moyes, ambaye aliitumikia timu hiyo miezi 10 akichukua nafasi ya kocha Sir Alex Ferguson.

Haijulikani kama Mholanzi huyo mwenye umri wa miaka 64 kama atashuhudia msimu wake wa mwishio Old Trafford, ingawa alisema kuwa anaamini ataendelea kuifundisha timu hiyo hadi atakapomaliza mkataba wake.

Baadhi ya mashabiki wa Man United wamemtaka kuondoka kocha huyo wazamani wa Ajax, Barcelona na Bayern Munich kuondoka, wakati baadhi yao wakizomea katika mchezo wa mwisho wakishinikiza aondoke katika mchezo dhidi Bournemouth.

Van Gaal anaweza kuiongoza Man United kutwaa taji lake kubwa la kwanza tangu mwaka 2013 taji la Ligi Kuu ya England chini ya Ferguson wakati Jumamosi 
watakapokabiliana na Crystal Palace katika fainali ya Kombe la FA kwenye Uwanja wa Wembley.

Lakini alikiri timu hiyo kumaliza katika nafasi ya tano ni sawa na hatua moja nyuma baada ya kuwaongoza Mashetani hao wekundu kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa katika msimu wake wa kwanza.
"Lengo letu katika mwaka wa kwanza na wa pili na watatu ni Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, alisema baada ya kushinda 3-1 dhidi ya Bournemouth.

"Ni kiwango cha juu na klabu kama Manchester United inatakiwa kucheza katika kiwango kama kile, lakini kuna klabu zaidi ambayo zinazotaka kucheza katika kiwango kile na hilo umeliona.

"Matarajio ni makubwa sana. Mashabiki wanatarajia mengi lakini nafikiri matarajio haya ni makubwa sana.