Wednesday, 16 December 2015

Eto'o apewa nafasi ya kuifundisha timu ya Uturuki ya Antalyaspor



ANKARA, Uturuki
NAHODHA wazamani wa Cameroon Samuel Eto'o (pichani), ameteuliwa kuwa kocha wa muda wa timu ya Uturuki ya Antalyaspor.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 34, aliyejiunga na  klabu hiyo Juni kwa mkataba wa miaka mitatu, amepewa mechi tatu za majaribio.

Mchezaji huyo amechukua timu hiyo kutoka kwa Yusuf Simsek, ambaye mkataba wake umesitishwa kwa makubaliano ya pande mbili tangy Desemba 7.

Antalyaspor itafanya uamuzi wa ama kumpa mkataba sa kufumi Eto'o baada ya mapumziko ya majira ya baridi.

Eto'o ataonozwa na kusaidiwa na Mehmet Ugurlu, ambaye ni mkurugenzi wa ufundi wa klabu hiyo, wakati Mcameroon huyo akipia hatua ya kwanza katika kazi yake hiyo ya uongozi.

Hatua hiyo haikutarajiwa kwa mchezaji huyo wazamani wa Barcelona, Inter Milan na Chelsea, ambaye amewahi kuihusisha na matukio kadhaa tata dhidi ya shirikisho la soka la nchi yake pamoja na wachezaji wenzake.

Mmoja kati ya wachezai wenzake wa kimataifa, Patrick M'boma, alikiri kuwa "alishtushwa na kitendo cha Eto'o kupewa haraka kazi hiyo ya uongozi.

Lakini alibainisha kuwa Eto'o, ambaye alicheza naye pamoa katika fainali mbili za Mataifa ya Afrika, alikuwa na mawazo ya muda mrefu kuhusu nafasi hiyo.

"Najua ilikuwa mipango yake kuwa kocha, aliniambia miaka mingi iliyopita, alisema M'boma.

"Lakini ninachoua hana uzoefu. Nategemea atakuwa kocha mzuri, lakini sijui.

Saturday, 12 December 2015

Jeshi Stars wajitoa mashindano ya netiboli ya Muungano yanayoanza Zanzibar Jumanne 2015



Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania Chaneta), Annie Kibira wakati wa mkutano mkuu wa TOC leo katika Kituo cha Amani Welezo, Zanzibar.
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
TIMU ya Jeshi Stars imejitoa kushiriki mashindano ya netiboli ya Muungano yanayotarajia kuanza Jumanne Desemba 15 kwenye Uwanja wa Gymkhana mjini Zanzibar.

Jeshi Stars ni miongoni mwa timu za Tanzania Bara zilizothibitisha kushiriki mashindano hayo kabla ya kujitoa katika dakika za mwisho kabisa za mashindano hayo.

Timu zingine za Bara zitakazoshiriki mashindano hayo ni pamoja na mabingwa Uhamiaji, JKT Mbweni, Polisi, Tumbaku ya Morogoro, Mbeya City ya Mbeya.

Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania Chaneta), Annie Kibira alisema jana mjini hapa, ambako anahudhuria mkutano mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) kuwa, alipewa taarifa juzi kuwa Jeshi Stars wamejitoa katika mashindano hayo.

Alisema kuwa anasubiri barua yao ili kujua sababu kamili iliyopelekea kujiondoa katika dakika za mwisho katika mashindano hayo.

Hatahivyo, taarifa zingine zinasema kuwa, timu hiyo imejiondoa baada ya baadhi ya wachezaji wake kwenda katika kozi ya kikazi.

Timu za Zanzibar zitakazoshiriki mashindano hayo ni JKU, Mafunzo, KBZ, Zimamoto, Chake Stars na Wete Stars.

Wakati huohuo, timu za Uhamiaji na JKT Mbweni zinatarajia kutua leo mjini hapa kwa ajili ya mashindano hayo.

Riadha Tanzania yawapiga pingu waandaaji wa Ngorongoro Marathon



Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
RIADHA Tanzania (RT) imezisimamisha mbio za Serengeti kwa muda usiojulikana baada ya kuwepo ubabaishaji mkubwa wakati wa kuendesha mbio hizo mwaka huu imeelezwa.

Kaimu katibu Mkuu wa RT, Ombeni Zavalla alisema jana kuwa, hatua hiyo ilifikiwa baada ya kikao kilichofanyika katikati ya wiki hii kati ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT), RT na waandaaji wa mbio hizo kujadili mapungufu yaliyojitokeza.

Zavalla alisema kuwa, wamezisimamisha mbio hizo baada ya kubaini mapungufu kibao yalijitokeza ikiwemo ubabaishaji katika zawadi, usimamizi na utawala, ambavyo navyo havikuwa sawa sawa.

Akifafanua mapungufu hayo, Zavalla alisema kwa upande wa zawadi waandaaji hao waliahidi kutoa sh.. milioni 1.5 kwa washindi wa kwanza na pili kwa wanawake na wanaume wakati washindi wa pili kila mmoa alitakiwa kupewa sh.milioni 1 na watatu sh. 500,000.

Lakini waandaaji hao walishindwa kutimiza ahadi hiyo kwa upande wa zawadi, ambapo washindi wote walipewa fedha pungufu tofauti na walivyoahidiwa.

Alisema pia waandaaji hao waliendesha mbio hizo bila ya kushirikiana na Chama cha Riadha cha Mkoa wa Simiyu, wanariadha walinusurika kugongwa na magari baada ya kutokuwepo kwa watu wa usalama na hakukuwa na wasimamizi wa kutosha na wenye uelewa wa mchezo huo.

Matatizo mengine yaliyoikeza ni pamoja na waandaaji wa mbio hizo kutosajiliwa na kuwashirikisha wanariadha kutoka nje ya nchi kama Kenya bila kuwaombea vibali RT.

Alisema ni kosa kubwa kwa waandaaji wa mbio kushirikisha wanariadha wa nje bila ya kuwaombea vibali kwa RT.

Aidha, BMT imeiagiza RT kukutana na waandaaji wote wa mbio hapa nchini na kuwapa mafunzo kuhusu taratibu zote za uandaaji wa mbio hizo ili kuepuka migogoro katika mbio wanazoandaa.

RISALA YA KATIBU MKUU WA TOC KWENYE MKUTANO MKUU WA KAWAIDA TAREHE 12/12/2015.



TANZANIA OLYMPIC COMMITTEE (TOC)
KAMATI YA OLIMPIKI TANZANIA

RISALA YA KATIBU MKUU WA TOC KWENYE MKUTANO MKUU WA KAWAIDA TAREHE 12/12/2015.

Ndugu Gulam Rashid, Rais, Kamati ya Olimpiki Tanzania, Ndugu Viongozi wa Serikali, Bara na Zanzibar,

Ndugu Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TOC,
Ndugu Wajumbe wa Mkutano Mkuu 2015, Wageni Waalikwa,
Waandishi wa Vyombo vya Habari, Mabibi na Mabwana:

Ndugu Rais,kwanza napenda nikushukuru ukiwa kama mwenyeji waMkutanohuukuwamgenirasmikutufunguliaMkutanohuuwamwakawakawaidawaKamatiyaOlimpiki Tanzania.

Ndugu Rais, walioko mbele yako niviongozi wa vyama vya Taifa zaidi ya 40 kutoka Zanzibar na Tanzania Bara wanaoongoza michezo Kitaifa.

Kwa heshima na taadhima, kwanza naomba kwaniaba ya Kamati ya Olimpiki Tanzania niwakaribishe rasmi kwenye Mkutano Mkuuhuuwamwaka 2015utakaoanzamudamfupikuanziasasabaadayaufunguziwako.

NduguWajumbe,MkutanoMkuuhuuambaoniwakawaidakikatiba, niwamuhimusananawapekeekwasababuunakamilisha mambo muhimu ya shughuli ambazo Kamati yenu imefanya kwa siku 365 zilizopita na kupanga kwakuthibitisha shughuli za TOC kwa siku zingine 365 zijazo.

Pia. Naomba nichukue nafasi kuwakaribisha wageni wetu wote waalikwa katika Mkutanohuu.Karibunisana.

Mhe.Rais,Mkutano unaofahari kuwa nawe kama mgenirasmi, jambo ambalo hatujazoea hasa ukiwa mwenyeji wa Mkutano huu.

NduguRaismwakahuuKamatiyaOlimpiki Tanzania imefanyashughulizakekamailivyokwenyeKalendaya 2015.

Moja ya shughuli hizo ni maandalizi ya timu yetu ya Vijana 4 (Ngumi na Riadha) iliyoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola kwa Vijana mjini Apia, Samoa.

Shughuli zingine ni kati ya zile 17 zilizo katika Mipango ya Olimpiki Solidariti.

Ndugu Rais, Ushiriki wa wanamichezo wetu umepungua sana kutokana na aidha vyama/Mashirikisho kutokuwa na wanamichezo wenyevi wango.

Mwaka 2016 Michezoya Olimpiki inategemea kufanyika mjini Rio de Jeneiro, Brazil.Ushiriki wa Tanzania katika Michezo hiyo umekuwa na mtihani mkubwa kwa vyama/mashirikisho yetu ya michezo kutofikia viwango vinavyotakiwa. Mpakasasa ndugu wajumbe, ni Riadha Tanzania (RT) pekee ambayo wanariadha wawili (2) mpaka sasa wamefikia viwango.

Kati ya Vyama/Mashirikisho ya michezo ambayo yalipendekezwa kujiandaa kwa michezo ya Rio 2016 ni Riadha Tanzania na Kuogelea ambao wameshiriki michezo yao ya dunia yanayoandaliwa na mashirikisho yao ya Kimataifa. Michezo mingine (Ngumi na Judo) hawakuweza kushiriki michezo yao ya Kimataifa.

Pamoja na kuwepo kwa mashindano ya Kimataifa ambayo vyama hivyo vinaweza kujaribu kufikia viwango bado vyama/mashirikisho hayo hayakuweza kuwasilisha mipango yao kwa Serikali na TOC kwa wakati muafaka ilikuona namna ya kuwasaidia.

Ndugu Rais wewe ni shahidi, mara nyingi wananchi wametoa lawama kwa Kamati ya Olimpiki Tanzania wanamichezo wetu wanapokosa medali au ushindi katika mashindano ya Kimataifa.
 BilanchikuwekezakatikamichezoVyamanaMashirikishoyaMichezoyataendeleakubebeshwalawamazakutoandaatimumapemainavyopasa.

Ndugu Rais, wewe nishahidi, viwango vya michezo vimepanda duniani.

Nchi nyingi duniani kwasasa vyama/mashirikisho yao ya michezo vimewekeza kwenye vijana wa umri mdogo wa chini (12),  mdogo (15) na mdogo kati (17). Lakini tukiulizana hapa tulipo ni vyama vingapi ambavyo vina mipango hiyo?

Tumekuwa na ukame wawanamichezo vijana, wakakamavu, na wenye vipaji vizuri ambao vinaweza kuanzishwa na kuendelezwa kuliwakilisha Taifa letu kwenye michezo ya Taifa na Kimataifa.

Bado michezo haichezwi katika Shule zetu, kuwepo kwa Umitashumta na Umisseta siyo ufumbuzi wa kutatua ukame wa wachezaji wa umri niliotaja hapo juu kama hakuna mipango mahususi ya kuwaendeleza vipaji vinavyopatikana wakati wa michezo hiyo. Bila kufanya hivyo michezo hiyo itakuwa kama tamashatu.

Majirani zetu na dunia kwaujumla wanapata vijana chipukizi mashuleni nakuwafundisha/kuwaendeleza hadi kufikia ngazi ya Kimataifa na kuwakilisha mataifa yao. Katika michezo niliyoitaja. Ni mategemeo yetu sote Serikali ya awamu ya tano ya Mhe. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itafanya mabadiliko makubwa katika tasnia hii ya michezo.

MwishonapendakutoashukraninyingikwabaadhiyaVyama/MashirikishoyetuyaMichezoyaTaifa (NSA/NSF) kwaushirikianowaliouonyeshakwamwakammojauliopita.

PianatoashukranikwaviongoziwamichezowaSerikalizetuzotembili Bara na Zanzibar kwaushirikianotuliokuwanaomudawote, halikadhalikaMashirikayaUmma, watubinafsi, namakampuni. UshirikianotulioupatakutokakwaoumesaidiasanaKamatiyaOlimpiki Tanzaniakutekelezawajibu wake. VilevileKamatiinatoashukranizakekwaOlimpikiSolidaritiambaokwakiasikikubwandiyoiliyosaidiakuendeshashughuliza TOC, ikiwapamojanakufanikishamkutanohuu.

Ahsanteni kwakunisikiliza.

Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kawaida wa Mwaka wa TOC unaofanyika leo Kituo cha Amani, Welezo Zanzibar

Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi akisoma taarifa yake ya mwaka katika Mkutano Mkuu wa TOC Kituo cha Amani Welezo, Zanzibar. Kulia ni Rais wa TOC Gulam Rashid na Mhazini msaidizi Juma Zaidi (kushoto).
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) wakati wa mkutano huo jana Zanzibar.
 







Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Gulam Rashid wakati wa ufunguzi  wa Mkutano Mkuu wa kawaida wa mwaka wa TOC unaofanyika leo Zanzibar. Kushoto ni Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi na Mhazini Mkuu Charles Nyange.




Mhazini Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Charles Nyange (kushoto) akipokea tuzo kwa niaba ya mmoja ya makampuni yaliyodhamini Siku ya Olimpiki.

Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TOC katika picha ya pamoja leo mjini Zanzibar.