Friday, 8 May 2015

Mwanariadha India afa kwa sumu, wengine hoi hospitalini



NEW DELHI, India
POLISI wa nchini India wanachunguza kifo cha mwanariadha wakike mwenye umri wa miaka 15 na wengine watatu wakinusurika kifo baada ya kula kile kinachodaiwa matunda yaliyowekwa sumu, alisema waziri.

Ilielezwa kuwa wanariadha 10 walikula `othalanga matunda pori, ambayo yaliwekwa katika vifungashio vyenye sumu katika kituo hicho cha michezo huko Alappuzha kusini ya jimbo la Kerala kinachoendeshwa na Mamlaka ya Michezo India (SAI).

Wanariadha hao walikutwa wakiwa wamepoteza fahamu katika hosteli yaol Jumatano jioni na walikimbishwa hospitalini ambako mmoja wao alifariki dunia huku wengine watatu wakiwa katika hali mbaya.

Wote wanne inaaminika kuwa walisaini taarifa ya kifo, walisema viongozi hao, lakini hakuna taarifa zaidi zilizotolewa kuhusu barua hiyo.

Walisema ni mapema mno kuhisi kuhusu kifo cha wanariadha hao chipukizi waliokuwa wakifanya mazoezi lakini ndugu wa waathirika hao walisema kuwa wasichana hao walikuwa wameathirika kiakili kutokana na kusumbuliwa na wanariadha wakubwa na makocha katika kituo hicho.

Waziri wa Vijana na Michezo Sarbananda Sonowal alisema polisi wanachunguza na Mkurugenzi Mkuu wa SAI alikuwa akiongoza taasisi hiyo pia.

"Sheria itachukua mkondo wake, lakini nakuhakikishia kuwa kama kuna mtu yoyote kutoka katika mamlaka ya michezo nchini India atapatikana na hatia kuhusiana na suala hili, atachukuliwa hatua za kisheria mara moja," alisema Sonowal katika taarifa yake.

Mkurugenzi Mkuu wa SAI Injeti Srinivas aliwaambia waandishi wa habari kuwa "ni tukio la kushtua sana ".

"Wasichana wanne walijaribu kujiua. Sasa tunataka kuwapatia vifaa vya bora vya afya, " alisema.

Gerrard amenifanya kuwa kocha bora-Mourinho



LONDON, England
KOCHA wa Chelsea Jose Mourinho anasema kuwa nahodha wa Liverpool Steven Gerrard amemfanya yeye kuwa "kocha bora", kabla ya timu hizo kukutana Jumapili kwa mara ya mwisho katika msimu huu wa Ligi Kuu ya England.

Mabingwa hao wapya wa England Jumapili wanawakaribisha Liverpool katika moja ya mechi za mwisho za Gerrard mwenye umri wa miaka 34 katika klabu hiyo yenye maskani yake Anfield. Mchezo huo unatarajia kuanza saa 11:00 jioni.

"Adui yangu, alinifanya kuwa kocha bora kwa sababu ilikuwa vigumu kumsimamisha, " alisema Mourinho, huku akiongeza kuwa alijaribu mara tatu kumsajili mchezaji huyo.

"Nasikitika sana hii ni mara ya mwisho nitakabiliana naye."

Gerrard alikaribia kusaini Chelsea wakati Mourinho alipoifundisha klabu hiyo kwa mara ya kwanza mwaka 2005, na kocha huyo Mreno alibainisha kuwa pia alimtaka mchezaji huyo akiwa Inter Milan na hata alipokuwa akifundisha Real Madrid.
 
Alisema kuwa amechelewa kumsajili mchezaji huyo kwa sasa kwani tayari klabu ya LA Galaxy ya Marekani imemuwahi: "Nimechelewa kumsajili. Hawezi kucheza dhidi ya Liverpool. Amefanya mambo makubwa akiwa Liverpool. Alikataa kabisa kuchezea klabu nyingine kubwa, ligi nyingine kubwa, aliamua kuichezea Liverpool pekee.

"Nani alijua kama siku moja nitacheza dhidi ya Steven kama kocha wa Liverpool?"

Endapo angemshawishi Gerrard kujiunga na the Blues, Mourinho alisema angekuwa amefanikiwa mchezaji huyo kumchezesha na Frank Lampard kitu ambacho makocha wengi wa England wanadaiwa kushindwa kukifanya.

Tuesday, 5 May 2015

Maoni ya makocha, viongozi kuhusu makundi Ligi ya Mabingwa Afrika



CAIRO, Misri
BAADA ya kupangwa kwa makundi ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika leo Jumanne, yafuatayo ni maoni ya viongozi na makocha wa timu zinazoshiriki hatua hiyo wakizungumza ratiba hiyo.

Hatem Abdel Gaafar (Timu Meneja, El Merreikh)
Ratiba ni nzuri na tunatarajia kufanya vizuri. Hii ni mara yetu ya pili kucheza hatua hii ya makundi. Lengo letu ni kutwaa ubingwa na hilo tutalifanyia kazi.

Wael Gomaa (Mkurugenzi wa Soka, Al Ahly)
Tulitarajia kupangwa dhidi ya timu ngumu, kutokana na ushiriki wa klabu zenyewe tangu mwanzo. Karibu klabu 10 angalau zimewahi kutwaa moja ya mataji ya Afrika huko nyuma.

Hivyo tulijua itakuwa ngumu kwetu kutetea taji tuliloshinda mwaka jana. Tuna wachezaji wazuri na kocha (Fathi Mabrouk) ambaye anaijua klabu vizuri sana.

Hamada Anwar (Timu Meneja, Zamalek)
Timu zote zilizofuzu ni mabingwa kutoka katika nchi zao. Natarajia tutakuwa na matokeo mazuri kutoka katika mchezo wa kwanza hivyo hatutakuwa katika presha katika mchezo wa marudiano.Tuna msimu mzuri na tunatarajia kushinda taji hilo.

Frederic Kitengie (Katibu Mkuu, TP Mazembe)
Ni ratiba nzuri kwetu. Katika kundi tuko na timu mbili zinashiriki kwa mara ya kwanza, ambazo ni Smouha na Moghreb Tetounae. Hizi zitatusumbua sana kwa sababu ni timu mpya hatuzijui vizuri.

Nimefurahi sana kuikwepa El Merreikh, ambayo inafundishwa na kocha wetu wazamani Diego Garzitto, ambaye anaijua vizuri timu yetu. Kundi jingine lina timu za Algeria dhidi ya Merreikh na ni vizuri tumeliepuka kundi kama hilo.

 Mohamed Ashraf (Rais, Moghreb Tetouane)
Ni vizuri tumezikwepa timu za Algeria. Ratiba inatupa nafasi angalau kucheza nusu fainali. Tunaangalia mbele kucheza na Smouha, kufuatia mapokezi mazuri tuliyoyapata wakati tumekwenda Misri kucheza dhidi ya Ahly.

Kwa sasa Sudan, nafikiri El Merreikh ni bora zaidi ya El Hilal, na hiyo itatuapa sisi nafasi. TP Mazembe ni timu imara sana katika kundi, lakini tuna nafasi.

Ratiba makundi Ligi ya Mabingwa Afrika yapangwa



 
CAIRO, Misri
KLABU tatu za Algeria zimepangwa katika kundi moja la michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya michuano hiyo kutokea kitu kama hicho.

Mabingwa watetezi Entente Setif watakutana na wenzao wa USM Alger na MC Eulma katika mechi za Kundi B, huku timu ya Al Merreikh ya Sudan ikikamilisha kundi hilo.

Nchi 12 za juu katika bara la Afrika kawaida hutoa timu mbili kila moja, lakini imekuwa tofauti kwa Algeria baada ya Entente Setif kushinda taji hilo mwaka jana, nchi hiyo ikapata nafasi nadra ya kuingiza timu tatu katika michuano hiyo msimu huu.

Ratiba hiyo ya makundi ilipangwa katika Makao Makuu ya Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) yaliyopo jijini hapa jana.

TP Mazembe Englebert ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ndio timu pekee iliyofuzu kwa hatua hiyo kutoka nje ya nchi za Afrika Kaskazini zinazozungumza Kiarabu, ikipangwa katika Kundi A.

Timu zingine zilizomo katika kundi hilo ni pamoja na Smouha (Misri), Moghreb Tetouan (Morocco) na Al Hilal (Sudan).

Mechi za hatua hiyo ya makundi zitaanza mwishoni mwa Juni huku timu mbili za kwanza kutoka kila kundi zitafuzu kucheza nusu fainali ya mechi mbili za nyumbani na ugenini Septemba na Oktoba.

Fainali ambayo itachezwa Oktoba na Novemba nayo itapigwa kwa mtindo wa mechi mbili za nyumbani na ugenini.

Ratiba kamili:

Kundi A: Smouha (Misri), Moghreb Tetouan (Morocco), TP Mazembe Englebert (DR Kongo) na Al Hilal (Sudan).

Kundi B: Entente Setif (Algeria, mabingwa watetezi), USM Alger (Algeria), Al Merreikh (Sudan), MC Eulma (Algeria)


Mahakama Burundi yamruhusu Pierre Nkurunziza kugombea urais



BUJUMBURA, Burundi
MAHAKAMA ya Kikatiba nchini Burundi imemruhusu rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu wa urais katika uchaguzi uliopangwa kufanyika baadae mwaka huu.

Kulingana na vituo vya redio nchini humo,Jaji wa mahakama hiyo alitoa uamuzi huo mapema leo asubuhi na kumruhusu rais huyo kuwania tena urais pamoja na vurugu zilizopo.

Jana jaji msaidizi wa mahakama hiyo Jaji Sylvere Nimpagaritse, alilitoroka taifa hilo akidai kuwa walikuwa wakishinikizwa kutoa uamuzi utakaompendelea rais Nkurunziza.

Rwanda imethibitisha kuwa jaji huyo yuko mjini Kigali nchini Rwanda ambako ametafuta hifadhi.

Kivazi cha Beyonce kilichotia fora