Tuesday, 19 September 2017
Kongamano la Kwanza Kitaifa la Usafiri wa Anga lafunguliwa Dar leo na Waziri Mbarawa
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (mwenye tai nyekundu waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano la Kwanza la Usafiri wa Anga linalofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Kushoto kwa Waziri ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Salim Msangi na kulia Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Bw. Hamza Johari.
Sunday, 17 September 2017
KMC yaanza vizuri LIgi Daraja la Kwanza Bara
TIMU ya soka ya Mawenzi Market ya Manispaa ya
Morogoro inayoshiriki kwa mara ya kwanza Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara imeshindwa
kutamba katika uwanja wake wa nyumbani baaada ya kufungwa na KMC ya Kindondoni,
Jijini Dar es Salaam kwa mabao 2-1.
Licha ya
kipindi cha pili Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini, Abdulaziz Abood
kuwaahidi wachezaji donge nono la Sh 800,000 endapo wangeshinda mchezo huo huku
ikiwa nyuma kwa bao 1-0 hadi mapumziko
ilishindwa kunyakua kitita hicho kwa
kupoteza mchezo huo kwenye uwanja wa nyumbani wa Jamhuri wa mjini Morogoro.
Bao la kwanza la Kinondoni ilipachikwa dakika ya nne
na mchezaji wa zamani wa timu ya Yanga
Stephen Mwasika na lilidumu hadi
mapumziko, ambbapo kipindi cha pili
dakika ya 51 vijana wa Mawenzi Market walisawazisha bao hilo kupitia mchezaji
Maulid Iddi kwa shuti hafifu baada ya mpira wa adhabu uliookolewa na beki wa
Kinondoni kumkuta mfungaji.
Timu ya Kinondoni ambayo ilikuwa na baadhi ya
wachezaji wenye uzoefu wa Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza ikiwa na Kocha Mkuu , Fred Felix Minziro ‘ Majeshi’ ilibadili mfumo wa uchezaji wa pasi fupi na
kutumia pasi ndefu uliowezesha kupata
bao la pili na la ushindi katika dakika ya 86 kupitia Cliff Athony baada ya
mpira uliopingwa na Mwasika kugonga mwamba na kumkuta mfungaji huyo.
Hadi dakika 90 za mchezo huo vijana wa KMC kutoka Kinondoni Jijini Dar es Salaam waliibuka kidedea kwa
ushindi wa mabao 2 -1 dhidi ya Mawenzi Market.
Mourinho aeleza siri United kumsajili Lukaku
LONDON, England
KOCHA Jose Mourinho anaamini Manchester
United ilimsajili Romelu Lukaku kwa sababu kwameweza kulipa fedha
kiasi cha fedha kilichotakiwa na Everton.
Man United walilipa kiasi cha fedha ambacho
kinaweza kuongezeka hadi pauni milioni 90 kswa ajili ya kumsajili mshambuliaji
huyo wa Ubelgiji,ambaye leo anatarajia kupangwa katika mchezo wa Super Sunday
dhidi ya Everton.
Lukaku mwanzo wake wa kucheza Old Trafford ulianza
kiaina, ambapo alifunga mabao sita katika mechi sita, wakati mshambuliaji
mwingine alikuwa katika mawindo ya United, lvaro Morata, alifunga mabao matatu
katika mechi nne za Ligi Kuu ya England akiwa na Chelsea.
The Blues (Chelsea) walilipa kiasi cha auni
milioni 6 kwa ajili ya kupata huduma ya Morata na Mourinho anahisi ni suala la
fedha tu wakati linaokuja suala la mipango ya kumsajili mshambuliaji huyo,
ambao klabu hiyo ilikua na kile muhimu kulipa kwa ajili ya kumsajili Lukaku.
"Sifikiri ni sababu ya ushawishi wangu,
hapana, " alisema Mourinho. "Nafikiri tulilipa fedha zilizoombwa na Everton
kwa ajili ya mchezaji huyo na mshahara ambao wakala wake aliuhitaji na tulimpa
wakala kamisheni aliyoitaka.
"Nafikiri hiyo ndio ilikuwa sababu
kubwa. Sioni sababu nyingine. Tulilia kile ambacho Everton walikuwa wakihitaji.
Klabu inayomuuza mchezaji ndio inaamua kiasi cha fedha ambacho klabu inayomtaka
mchezaji inatatakiwa kulia au kutoliap.
Saturday, 16 September 2017
Ismail Juma avunja rekodi ya nusu marathoni
Na Mwandishi Wetu
Mwanariadha Ismail Juma (pichani) leo Jumamosi ameweka rekodi mpya ya taifa ya Tanzania
ya mbio za kilometa 21 au nusu marathoni.
Mtanzania huyo aliweka rekodi hiyo mpya ya taifa kwa kukimbia kwa
muda wa dakika 59:30 katika mbio zilizofanyika Jijini Mattoni, Jamhuri ya
Czech.
Rekosi ya zamani ya taifa ya dakika 59:52 ilikuwa ikishikiliwa na
Dickson Marwa aliyoiweka Februari mwaka 2008 Abu Dhabi, Falme za Kiarabu.
Manchester City yaikandamiza Watford mabao 6-0
LONDON, England
SERGIO Aguero
amefunga mabao matatu au `hat-trick’ wakati Manchester City ikishika usukani wa
msimamo wa Ligi Kuu ya England leo baada ya kutoa kichapo kikali cha mabao 6-0 kwa Watford.
Awali, Watford
ambao ilikuwa haijafungwa nayo pia ingeweza kuongoza msimamo wa ligi hiyo
endapo ingekifunga kikosi cha kocha Pep Guardiola, lakini kilishindwa kufanya
hivyo.
Kikosi cha Man
City sasa kimeshinda mechi tatu na kufunga jumla ya mabao 15.
Watford baada ya
kipigo hicho imebaki na pointi zake nane na kuangukia katika nafasi ya 10 ya
msimamo wa ligi hiyo inayoshirikisha jumla ya timu 20.
Katika mechi
zingine leo; Crystal Palace ilipokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa
Southampton, huku Huddersfield Town ikitoka sare ya 1-1 na Leicester City na
Liverpool ilibanwa na Burnley kwa sare ya 1-1.
Mechi nyingine leo, Newcastle United
iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Stoke City, West Bromwich Albion
ilitoka suluhu na West Ham United.Wakati huohuo, Chelsea kesho itacheza na Arsenal wakati Manchester United watakwaana na Everton kwenye Uwanja wa Old Trafford.
MSIMAMO LIGI KUU ENGLAND
| Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
| 1 | Manchester City | 5 | 4 | 1 | 0 | 16 | 2 | 14 | 13 |
| 2 | Manchester United | 4 | 3 | 1 | 0 | 12 | 2 | 10 | 10 |
| 3 | Chelsea | 4 | 3 | 0 | 1 | 8 | 5 | 3 | 9 |
| 4 | Newcastle United | 5 | 3 | 0 | 2 | 6 | 4 | 2 | 9 |
| 5 | Huddersfield Town | 5 | 2 | 2 | 1 | 5 | 3 | 2 | 8 |
| 6 | Burnley | 5 | 2 | 2 | 1 | 6 | 5 | 1 | 8 |
| 7 | Liverpool | 5 | 2 | 2 | 1 | 9 | 9 | 0 | 8 |
| 8 | Southampton | 5 | 2 | 2 | 1 | 4 | 4 | 0 | 8 |
| 9 | West Bromwich Albion | 5 | 2 | 2 | 1 | 4 | 4 | 0 | 8 |
| 10 | Watford | 5 | 2 | 2 | 1 | 7 | 9 | -2 | 8 |
| 11 | Tottenham Hotspur | 4 | 2 | 1 | 1 | 7 | 3 | 4 | 7 |
| 12 | Arsenal | 4 | 2 | 0 | 2 | 7 | 8 | -1 | 6 |
| 13 | Stoke City | 5 | 1 | 2 | 2 | 5 | 6 | -1 | 5 |
| 14 | Leicester City | 5 | 1 | 1 | 3 | 7 | 9 | -2 | 4 |
| 15 | Brighton & Hove Albion | 5 | 1 | 1 | 3 | 4 | 7 | -3 | 4 |
| 16 | Swansea City | 4 | 1 | 1 | 2 | 2 | 5 | -3 | 4 |
| 17 | Everton | 4 | 1 | 1 | 2 | 2 | 6 | -4 | 4 |
| 18 | West Ham United | 5 | 1 | 1 | 3 | 4 | 10 | -6 | 4 |
| 19 | AFC Bournemouth | 5 | 1 | 0 | 4 | 3 | 9 | -6 | 3 |
| 20 | Crystal Palace | 5 | 0 | 0 | 5 | 0 | 8 | -8 | 0 |
Subscribe to:
Posts (Atom)









