Wednesday, 26 October 2016

Serikali yazipiga stop Yanga, Simba kuendelea na michakato ya kubadili umiliki wa klabu hizo



Kaimu Katibu Mkuu wa Barraza la Michezo la Taifa (BMT), Mohamed Kiganja (kulia) akimkabidhi zawadi kocha mkuu wa timu ya taifa ya riadha iliyoshiriki Michezo ya Olimpiki ya Rio 2016, Francis John. Wapili kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Riadha Tanzania (RT), Rehema Killo na aliyekuwa kiongozi wa msafara wwa timu ya Tanzania ya Olimpiki, Suleiman Jabir. 

Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imezipiga stop Yanga na Simba kuendelea na michakato yao ya kubadili umiliki wa klabu hizo hadi pale yatakapofanyika marekebisho ya katiba zao.

Hayo yalitangazwa leo na Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Mohamed kiganja wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Kiganja alisema kuwa Serikali haikatai mabadiliko ya uendeshaji katika klabu hizo pamoja na zingine za wanachama, ila inachotaka kwanza kufanyike marekebisho ya katiba zao, ambayo sasa hayaruhusu mabadiliko hayo.

Alisema kuwa BMT inapenda kuona kwamba wahusika wanafuata sheria na taratibu za nchi katika kufikia malengo yao, ambapo alisisitiza kuwa kuendelea na michakato hiyo kabla ya kurekebisha katiba zao ni kosa na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Hivi karubuni kumeibuka michakato ya watu wakitaka kubadilisha umiliki wa klabu za wanachama na kuzielekeza katika utaratibu wa hisa na ukodishwaji, vitendo vimesababisha migogoro mikubwa ambayo inaashiria uvunjifu wa amani…”

Kiganja alisema tayari mezani kwake kuna barua kibao za wanachama wa Yanga wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato huo wa kubadilisha umiliki.

Ibara ya 56 ya Katiba ya Yanga iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 inaeleza kuhusu kampuni ya umma:

Inaeleza kuwa kutakuwa na kampuni itakayojulikana kama Young African Sports Corporation Limited ambayo itasajiliwa chini ya sheria ya makampuni kama kampuni ya umma yenye hisa.

Sehemu ya pili ya ibara hiyo inasema wanachama wote katika klabu ambao katika tarehe ya marekebisho ya Katiba ya mwaka 2007 wako hai watakuwa,kwa nguvu ya uanachama wao, wanahisa katika kampuni kwa kiwango cha idadi ya hisa watakapopata kwa mujibu wa muafaka wa Yanga uliofikiwa na Wana Yanga Juni 22, 2006.

Klabu itamiliki hisa zilizosawa na asilimia 51 ya hisa zote zilizomo katika klabu hiyo.

Mkutano Mkuu wa Uchaguzi utachagua wanachama wawili, ambao sio miongoni mwa viongozi wa klabu kuwa wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni kwa ajili ya kuwakilisha maslahi ya klabu kwenye kampuni.

Tayari Yanga iko chini ya Kampuni ya Yanga Yetu ambayo ni mali ya mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji, ikiwa ni kinyume na katiba yao wenyewe.

Kiganja alisisitiza kuwa klabu zisitishe mipango ya kubadilisha uendeshaji na ziendelee kuwa mali ya wanachama.
Wakati Yanga walikuwa tayari wameishaingia mkataba wa miaka 10 wa kuikodisha klabu yao, wenzao wa Simba walijipa miezi sita kukamilisha taratibu za kuuza hiza.

Tuesday, 25 October 2016

SAMAKI AINA YA NYANGUMI ALIVYOPATIKANA KILWA MASOKO NA KUNUFAISHA WATU

Watafiti wakipima mabaki ya samaki mkubwa aina ya nyangumi katika ufukwe wa bahari ya Hindi, Kilwa Masoko, ambaye anadaiwa kuwa ni mkubwa miongoni mwa waliowahi kuonekana nchini.
Sehemu ya tumbo na mbavu za nyangumi huyo mwenye uzito wa tani karibu 40 na urefu wa mita 41.
Mtoto Jumanne akichota mafuta kutoka katika mabaki ya samaki aina ya nyangumi katika ufukwe wa bahari ya Hindi Kilwa Masoko mkoani Lindi hivi karibuni. Mafuta hayo alikuwa akiyauza kwa sh. 5,000  kwa chupa akidai yanatibu magonjwa mbalimbali.

Monday, 24 October 2016

Ukiwa na Vigezo hivi unaweza kuwa kiongozi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC)



22.0   TOC LEADERSHIP QUALITIES AND QUALIFICATIONS

In order to qualify for election of the Executive Committee of TOC the candidates must prove that they understand and have extensive knowledge of TOC constitution, its institutions, its activities and operations

                  Candidate must:

22.1 Be a citizen of the United Republic of Tanzania who has attained the age of twenty one

22.2 Have an acceptable sound discipline and be a person of good behaviour in the society

22.3 Have at least an O Level Secondary School Education with a proven track record in Sports Administration

22.4 Have a thorough knowledge of the Olympic Movement

22.5 Have a reasonable experience in sports leadership at a national or international level

22.6 Have been a sports leader as NSA or any other Sports Body which have a national outlook and has attended some leadership seminars and  courses.

22.7 Have ability to speak fluently both English and Kiswahili languages

22.8 Not be serving a suspension by TOC, any NSA, club or and international sports body

22.9 Be committed and ready to dispose freely a minimum of thirty (30) days per year in separate periods to accomplish the Executive Committee duties

        22.10 Be honest and impartial

Fomu za kuwania uongozi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) kuanza kutolewa kesho jijini Dar es Salaam na Zanzibar


Rais wa Kamati ya Olimpiki, TOC, Gulam Rashid akizungumza hivi karibuni. Kushoto ni Katibu Mkuu wake, Filbert Bayi.

Na Mwandishi Wetu
MBIO za kuwania uongozi katika Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) zinatarajia kuanza kesho Jumanne Oktoba 25 wakati fimu za kuwania uogozi zitakapoanza kutolewa tayari kwa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Dodoma Desemba 10 mwaka huu.

Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi alisema jijini Dar es Salaam wiki iliyopita kuwa, fomu hizo zitaanza kutolewa Oktoba 25 na mwisho wa kurejeshwa ni Novemba 15 saa 10:00 jioni katika ofizi za kamati hiyo zilizopo Mwananyamala na ofisi ndogo ya Zanzibar.

Bayi alisema kuwa fomu za wanaotaka kugombea Urais, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mhazini Mkuu, Mhazini Msaidizi wachukua fomu kwa sh. 200,000 kila mmoja huku wanaotaka kuwania ujumbe watatakiwa kutoa sh 150,000.

Kamisheni ya Uchaguzi itakutana jijini Dar es Salaam na kuhakiki fomu zote Novemba 18 kabla ya kufanyika kwa usaili utakaendeshwa Novemba 22 jijini Dar es Salaam wakati Zanzibar utakuwa Novemba 24.

Alisema kuwa usaili huo utafanyika kwa lugha ya Kiswahili na kiingereza, kwani ndizo lugha za TOC, ambapo Bayi alisisitiza kuwa wagombea wanatakiwa kujua vizuri kugha hizo.

Alisema kuwa kila mgombea atakayepitishwa kugombea nafasi yoyote ya uongozi ambaye sio mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TOC, atatakiwa kujigharamia zote za kwenda Dodoma, malazi na chakula akiwa huko.

Kamisheni ya Uchaguzi inaoongozwa na Lloyd Nchunga na Harrison Chaula (Tanzania Bara) na Abdallaj Juma Mohamed (Zanzibar).

Aidha, Bayi alisema kuwa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania (Kawata) itafanya uchaguzi wake mjini Dodoma Desemba 6 siku mbili kabla ya ule wa TOC katika Hotel ya Dodoma.